• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

RC MAKALLA AAGIZA MAENEO YA TAASISI KUWEKEWA MIPAKA

Posted on: October 19th, 2023

Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela imetakiwa kuhakikisha inayapima maeneo yote ya taasisi za umma ikiwemo vituo vya afya shule kwa kuziwekea vigingi sambamba na kuziwekea uzio, ili kuepukana na migogoro ya ardhi na uvamizi wa wananchi katika maeneo hayo , kwani ardhi haiongezeki ila watu wanaongezeka

Maagizo hayo yametolewa na Mhe CPA Amos Makalla, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza alipofika katika shule mpya ya sekondari katika kata ya kiseke kwa ajili ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa shule mpya hiyo ya kimkakati akiwa katika muendelezo wa ziara ya siku mbili ya kusikiliza kero za wananchi na ukaguzi wa miradi ya maendeleo.


“Ipo haja ya kuhakikisha maeneo yote ya umma yanalindwa na kutunzwa, kwani ardhi haiongezeki ila watu wanaongezeka na watu wa siku hizi hawaogopi kuvamia maeneo ya umma, tuyapime maeneo yetu ikibidi tuyawekee na uzio”. Alisema RC Makalla


Aidha Mhe Makalla mbali na kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hasan kwa kutoa fedha za ujenzi wa shule hiyo ameitaka Manispaa ya Ilemela kuacha kujenga majengo ya mtawanyiko badala yake ijenge kuelekea juu (maghorofa) ili kutumia sehemu ndogo ya ardhi na kuwa na mpango bora wa matumizi ya ardhi.


“Tunapoletewa fedha tujipange kujenga majengo ya ghorofa mwanza haina maeneo mengi ya tambarare ya kujenga miundombinu ya huduma za jamii”, alisema RC Makalla


Mhe. Ramadhan Mwevi ni  Diwani wa Kata ya Kiseke, amemshukuru Mhe Rais kwa kutoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa shule ya kimkakati katika kata hiyo huku akibainisha umuhimu wa uwepo wa shule hiyo ambapo amesema ujenzi wa shule hiyo utakapokamilika utasaidia kuondoa adha ya wanafunzi kutembea umbali mrefu.


Sambamba na hilo, Mhe Mwevi amesema kuwa kupitia ujenzi wa shule hii ajira mbalimbali zimepatikana ambapo jumla ya mafundi wakuu 7, mafundi wasaidizi 25 na wastani wa vibarua 40 kwa siku wamepata ajira. Pia Mradi umetoa ajira kwa Mama lishe na watoa huduma wengine ambapo wengi wao ni wakazi wa Kata ya Kiseke.


Akisoma taarifa ya mradi Mwalimu Albert Munale ambae ni meneja mradi amesema kuwa kukamilika kwa mradi huu kutaondoa changamoto ya mrundikano wa wanafunzi katika Kata ya Kiseke pamoja na Kata za jirani za Ilemela, Nyasaka, Kawekamo, Kahama na Buswelu kwa kuwa baadhi ya wanafunzi wa shule ya Angelina Mabula watahamishiwa shule mpya na kuongeza ufanisi.


Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela ni kati ya Halmashauri zilizoidhinishwa fedha za ujenzi wa sekondari mpya kupitia Mradi wa SEQUIP kwa mwaka wa Fedha 2022/2023 ambapo ilipokea fedha kutoka Serikali Kuu kiasi cha shilingi milioni 584.28






Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.