• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

Posted on: May 5th, 2025

“Nitoe rai kwa wazazi na wananchi waendelee kuwafichua watoto wenye mahitaji maalum ili na wao wapate haki yao ya msingi ya elimu, kwani baadhi ya wazazi wamekuwa wakiwaficha watoto wao nyumbani. Niwahikikishie kuwa kwa sasa shule zetu zina mazingira mazuri na rafiki kwa ajili ya watoto hao kusoma na kujifunza”

 

Rai hiyo imetolewa na mkuu wa divisheni ya elimu ya awali na msingi Mwalimu Mashelo Bahame, wakati wa mapokezi ya vifaa vya wanafunzi wenye mahitaji maalum kwa ajili ya shule za msingi za manispaa ya ilemela zenye watoto hawa kutoka serikali kuu kupitia Ofisi ya Rais TAMISEMI siku ya Jumatatu ya tarehe 05 Mei 2025.

 

Pamoja na rai hiyo Mwalimu Mashelo amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kwa namna ambavyo ameendelea kupambania elimu ya watanzania kwani pamoja na vifaa hivyo takriban shilingi milioni 180 zimeshatolewa na serikali kwa ajili ya ujenzi wa bweni la Watoto wenye mahitaji maalum ambalo limekamilika likiwa na uwezo wa kubeba wanafunzi 80

 

Mwalimu Amiri Biliomo kutoka shule ya msingi ya Lake View ametoa shukran zake kwa serikali kwa kuwafikiria wanafunzi hao wenye mahitaji maalum kwani vifaa hivyo vitaenda kuwasaidia katika masomo yao.

 

“Kiukweli hili ni jambo jema na sisi kama wadau wa elimu tunaiomba serikali iendelee kutoa vifaa hivi kwa watoto hawa ili kuboresha mazingira yao ya kujifunzia na kufundishia” amesema Mwalimu Amiri.

 

Mwalimu Regina Manyama wa shule ya msingi Ibeshi yenye elimu maalum, ameshukuru kwa vifaa hivyo ambavyo vinaenda kuwarahisishia kazi ya kufundisha katika shule yao ameongeza kusema hii ni mara ya tatu kupokea vifaa hivyo vya Watoto wenye mahitaji maalum.

 

“Tunaishukuru serikali kwa kuendelea kututhamini na nitasoma kwa bidii ili nami nije niwasaidie wenzangu wenye uhitaji” Ni kauli ya Fatuma Haji mwanafunzi wa darasa la saba katika shule ya msingi Lake View  

 

Nae Elisha Ezekiel, anaesoma shule ya msingi Ibeshi darasa la saba ameishukuru serikali na kuomba kuendelea kupatiwa vifaa hivi ili waweze kusoma vizuri

 

Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela imeendelea kupokea vifaa hivi vya wanafunzi wenye mahitaji maalum kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa lengo la kuwaboreshea mazingira ya kujifunzia na kufundishia na hii ikiwa ni mara ya pili katika mwaka wa fedha 2024/2025. Vifaa vilivyopokelewa ni pamoja na mafuta, miwani, kofia kwa ajili ya wanafunzi wenye ualbino pamoja na vifaa vingine kama fimbo kwa watoto wenye ulemavu wa kuona, vifaa vya kurekodi na vingine vinavyotumika na watoto wenye mahitaji maalum.

 

                                                



Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.