• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

'PIKIPIKI ZIKALETE MATOKEO CHANYA KATIKA SEKTA YA KILIMO', KITINGA AELEKEZA

Posted on: February 9th, 2023

Katibu Tawala wa Wilaya ya Ilemela, Ndugu Said Kitinga amewataka maafisa ugani kuhakikisha kuwa pikipiki walizopatiwa zinaenda kuleta matokeo chanya katika sekta ya kilimo ikiwa ni pamoja na kuzitumia kwa malengo mahususi ambayo ni kukuza kilimo kwa asilimia 10 kufikia mwaka 2030.


Akikabidhi pikipiki hizo kwa maafisa ugani kilimo 38 Ndugu Kitinga amewataka kuwafikia wakulima sehemu zote, jambo ambalo llitawasaidia na kuwainua vijana waliojiajiri katika kilimo kwa kuwapatia maarifa juu ya masuala mbalimbali ya kilimo ikiwa ni pamoja kufanya kazi kwa ueledi.

“Pikipiki hizi ni nyenzo muhimu katika moja ya vifaa mnavyovihitaji na zitawasaidia katika kuwafikia wananchi popote walipo ili kuwafundisha kilimo cha kibiashara na mwisho wa siku waweze kufanya kazi kwa tija”, amesema Ndugu Kitinga


Mhe Rais wakati anakabidhi vifaa hivi pale Dodoma aliwataka mtakapokabidhiwa pikipiki hizi muende mkazitunze na kuzitunza si kuziweka ndani bali ni kuzifanyia matengenezo kwa wakati huku akiwataka kmkazitumie kwa malengo mahususi ambayo yamekusudiwa ya kuwafikia wananchi katika maeneo yenu ya kazi” alinukuu Ndugu Kitinga


Aliongeza kusema kuwa ni matumaini yake kuwa kupatikana kwa pikipiki hizi kutasaidia kuwainua vijana ambao wamejiajiri katika suala la kilimo ili waweze kupata maarifa na kuweza kuwavutia  vijana wengi kuingia katika shughuli za kilimo na mwisho wa siku watafanya shughuli zao kitaalamu zaidi na watainua uchumi wao pamoja na kujiajiri.


Akimkaribisha Katibu Tawala, mkurugenzi wa Manispaa Mhandisi Modest Apolinary, amewataka maafisa ugani hao kuhakikisha pikipiki hizo zinaenda kuwasaidia wakulima katika maeneo yote ambao yalikuwa hayafikiki kwa wakati na kuwataka kuanza kazi mara moja.

Neema Semwaiko ni Mkuu wa Divisheni ya kilimo ,mifugo na uvuvi na pia ni afisa kilimo Manispaa ya Ilemela pamoja na kumshukuru Mhe Rais kwa kuwafikia amemshukuru pia waziri wa kilimo ambae amesaidia upatikanaji wa pikipiki hizi na kusema kuwa ni jambo la kihistoria.


“Binafsi nimefanya kazi zaidi ya miaka 30 lakini tulikuwa hatujawahi kupata pikipiki kwa mkupuo kama tulivyopata hivyo tunamuahidi Mhe Rais kwamba hizi pikipiki tunaenda kuzitumia kwa malengo husika, tutaongeza uzalishaji na tutazitumia kwa ukamilifu kwa kuwafikia wakulima wengi zaidi ili kuweza kuongeza uzalishaji ili kufikia lengo la serikali kwamba kufikia 2030 kilimo kiwe kimekua kwa asilimia kumi”, amesema Bi Semwaiko

Nae Tumaini Lushinde afia kilimo kata ya Sangabuye kwa niaba ya wenzake ameahidi kuvitunza vifaa hivi  na kusema kuwa vitaleta tija upande wa kilimo hususan kwa kuwatembelea wakulima na  kuwapa mbinu za kilimo bora akiahidi kutoka hapo walipo na kufika katika kiwango kilichokusudiwa  kwa ajili ya kuweza kuwainua wakulima.


Jumla ya pikipiki 38 zimekabidhiwa kwa maafisa ugani kilimo 38, kutoka serikali kuu kupitia wizara ya kilimo kwa ajili ya kutekeleza shughuli mbalimbali za sekta ya kilimo.


Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.