• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

NAIBU WAZIRI OR-TAMISEMI AIPONGEZA ILEMELA KWA MUITIKIO WA WANANCHI KATIKA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

Posted on: February 27th, 2020

Naibu Waziri OR-TAMISEMI, Mhe. Josephat Kandege (Mb), ameipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela kwa muitikio wa wananchi katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuzitaka halmashauri zingine kuja kujifunza namna ambavyo halmashauri imeweza kuwaleta wananchi pamoja  na kuweza kushirikiana nao katika suala zima la maendeleo.


 “Nitoe wito kwa halmashauri zingine kuja kujifunza namna ushirikiano huu umewezakana kwani mwitiko wa wananchi umekuwa mkubwa sana katika kutekeleza miradi ya maendeleo hususani ujenzi wa vyumba vya madarasa  pamoja na miradi mingine inayojitokeza. Niwasihi wananchi kuendelea kujitoa katika suala zima la maendeleo kwani maendeleo ni ya kwetu sote”, Alisisitiza


Mhe. Kandege aliyasema hayo alipokuwa katika ziara ya kikazi kwa ajili ya kutembelea na kukagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela ambapo pia alipata fursa ya kuzungumza na watumishi wa manispaa.

Akiongea na watumishi aligusia suala la elimu ambapo aliipongeza Halmashauri kwa kushika nafasi ya pili kitaifa katika matokeo ya darasa la saba kwa mwaka 2019. Huku akiwaelekeza Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi kuhakikisha kuwa watoto wote waliofaulu wanaingia kidato cha kwanza na iwapo watakuwepo watoto ambao hawajaripoti basi wazazi wa watoto hao wakamatwe.

Pia alitoa pongezi kwa Halmashauri kwa kupata hati safi mara tano mfululizo na kusema kuwa halmashauri yoyote inayopata hati safi ni wazi  kuwa mkaguzi wa ndani anatekeleza majukumu yake ipasavyo na pia Mkurugenzi anakuwa anajitambua kwani anakuwa anafuata ushauri wa mkaguzi wa ndani .


Mhe Kandege aliendelea kusema kuwa ameridhishwa na utekelezaji mzuri wa miradi ya maendeleo kwani hakuna mradi ambao ametembelea hajaridhika nao huku akielekeza masuala mbalimbali hususani suala la utoaji mikopo ambapo alielekeza kuwa, halmashauri ihakikishe kuwa inatenga pesa ya kutosha na kutoa pesa ya kiwango kikubwa ili kuviwezesha vikundi hivyo kutekeleza miradi mikubwa yenye kuleta tija na kuweza kuondoa hali duni ya maisha kwa wananchi wa Ilemela.


Ameyasema hayo alipotembelea kikundi cha wanawake ambacho kinapata mkopo kutoka Ilemela ambapo alishauri kuwa pindi watakapomaliza mkopo walionao Mkurugenzi ahakikishe anawapa mkopo wa Mil 20 ili kuwawezesha kufanya ujasiriamali wa kiwango kikubwa.


Sambamba na hilo alitoa maelekezo akiwa katika shule ya sekondari ya Buswelu na kumuelekeza mkurugenzi kuhakikisha kuwa anakamilisha kazi zilizobakia ili kuwawezesha wanafunzi kusoma katika mazingira mazuri.

Nae Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela, Ndugu John Wanga alimshukuru Naibu Waziri kwa kutembelea halmashauri yake  na kuahidi kutekeleza maelekezo yote aliyoyatoa kwani jukumu kubwa ni kuhakikisha kuwa miradi inatekelezwa ili kuweza kuwaondolea wananchi  adha mbalimbali,  huku akimshukuru Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuipatia pesa  Manispaa ya Ilemela kwa ajili ya kutekeleza mradi mkubwa wa kimkakati wa stendi ya mabasi na eneo la uegeshaji wa malori kwani mradi utakapokamilika utaongeza mapato kwa Halmashauri.


Akiwa katika Manispaa ya Ilemela Mhe. Josephat Kandege alikagua miradi ya ufyatuaji wa matofali unaomilikiwa na halmashauri, shule ya Sekondari Buswelu, mradi wa barabara ya Sabasaba-Kiseke-Buswelu na barabara ya Makongoro junction-Mwaloni. Pia alipata fursa ya kukagua kikundi cha wanawake wanaopata mkopo toka halmashauri, pamoja na mradi wa kimkakati wa ujenzi wa stendi ya mabasi na maegesho ya malori uliopo Nyamhongolo.





Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.