• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

MSIONE AIBU KUJIUNGA NA ELIMU YA WATU WAZIMA-LALIKA

Posted on: September 15th, 2020

Mhe. Dkt Severine Mathias Lalika, Mkuu wa Wilaya ya Ilemela amewataka  wananchi wa Ilemela kutokulionea aibu suala la kujiunga na elimu ya watu wazima.

Ameyasema hayo katika maadhimisho ya juma la elimu ambalo huadhimishwa kuanzia  tarehe 01 hadi tarehe 08 mwezi wa tisa ya kila mwaka.


“Wananchi msione aibu kujifunza, Halmashauri yetu inao mfumo mzuri wa utoaji wa elimu kwa watu wazima. Na ni jukumu letu sote kuhamasisha wahitaji wa elimu ya watu wazima kujiunga na mipango mbalimbali inayoendelea kufanya kazi ndani ya Halmashauri ikiwa ni pamoja na Mpango wa uwiano kati ya elimu ya watu wazima na jamii (MUKEJA),Mpango wa elimu ya Msingi kwa walioikosa (MEMKWA),Elimu Masafa na Masomo ya ana kwa ana -Open and Distance Learning(ODL) na elimu ya ufundi.Tusiogope tuchangamkie fursa zilizopo kwa manufaa ya jamii yetu” alisema .


Aidha alisema kuwa wilaya yake inatambua uwepo wa watu wazima wasiojua kusoma na kuandika na kumtaka Mkurugenzi wa Manispaa kuendelea na mikakati ya kuhakikisha watu wake wote wanajua kusoma na kuandika kupitia njia mbalimbali za kutoa elimu kwa njia rahisi ili watu wazima waweze kuelewa na kujifunza haraka.


“Katika nyakati hizi nchi zote duniani ikiwemo Tanzania, zinafanya bidii kuhakikisha watu wake wote wanapata elimu iliyo bora bila kujali jinsia kwa kuwa elimu ni moja ya haki za msingi za binadamu. Elimu inawasaidia wanadamu kuendana na mabadiliko yanayotokea hapa duniani”.Alisisitiza


Nae Mkuu wa idara ya elimu msingi katika Manispaa ya Ilemela Ndugu Isack Busungu amesema kuwa elimu haina mwisho na ni muhimu watu wote kupata elimu ya utambuzi wa vitu mbalimbali katika maisha ya kawaida ya mwanadamu.

Pamoja na hayo alisema kuwa Manispaa ya Ilemela inaendelea kusimamia masuala mbalimbali ya mpango wa elimu kwa walioikosa (MEMKWA), mpaka sasa manispaa ina jumla ya wanafunzi 977 ambapo wavulana ni 535 na wasichana 442, kati yao jumla ya wanafunzi 79 wamehitimu elimu ya msingi 2019 na kuingia kadato cha kwanza 2020 ambapo wavulana ni 45 na wasichana ni 34.


Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela imeungana na Halmashauri zingine nchini katika kuadhimisha juma la elimu ya watu wazima linaloadhimishwa kila mwaka tarehe 01 hadi 08 Septemba duniani mwaka huu iliyobebwa na kauli mbiu ‘Elimu ya watu wazima ituwezeshe kuwachagua viongozi bora watakao tuletea maendeleo’.


Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.