• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

MKURUGENZI WAYAYU ATOA MOTISHA KWA WATUMISHI KITUO CHA AFYA BUZURUGA

Posted on: October 23rd, 2024

Watumishi wa kituo cha afya Buzuruga wamepewa motisha ya kiasi cha shilingi laki tano kama ishara ya kutambua, kuthamini na kupongeza kazi nzuri wanazozifanya katika kuwahudumia wananchi .

Akizungumza katika kikao chake na watumishi wote wa idara ya afya manispaa ya Ilemela katika kituo cha afya Buzuruga mkurugenzi wa manispaa ya Ilemela Bi. Ummy Mohamed Wayayu amewapongeza watumishi wa kituo hicho pamoja na kuwasisitiza kuendelea kufanya kazi kwa bidii bila kujali maslahi  binafsi kwa kuwa kazi wanayoifanya ni ya wito wa ki Mungu .

"... Inawezekana mkafanya kazi wengi alafu akatambulika mmoja wenu, Hiyo isiwavunje moyo sifa ya taasisi huwa ni ya wote, mie kama mkurugenzi wenu nitawapa laki tano tufanye kazi raha ya kufanya kazi kwa bidii siku zote huwa inalipa..." alisema

Aidha Bi.Wayayu ameahidi kuzifanyia kazi changamoto zote zilizowasilishwa na wataalam wa kituo hicho cha afya ikiwemo upungufu wa afisa tehama wa kituo na afisa ugavi ili kuongeza ufanisi wa kazi katika kituo hicho .

Kwa upande wake mganga mkuu wa wilaya ya Ilemela Daktari Maria Kapinga mbali na kumshukuru mkurugenzi huyo kwa namna anavyounga mkono juhudi za watumishi wa idara ya afya amewataka watumishi wachache wa kituo hicho wanaolalamikiwa na baadhi ya wananchi kuongeza juhudi na uzalendo katika kazi ili kuendelea kukipatia sifa kituo hicho pamoja na kuondoa malalamiko kwa wananchi .

Suleiman Baruani ni muhasibu wa kituo hicho ambapo ameomba kujengewa uwezo juu ya mifumo mipya ya fedha na ugavi ili kurahisisha utoaji huduma kwa wananchi wakati mganga mfawidhi wa kituo hicho Dkt. Ndinginya akiomba kuongezwa kwa majengo ili watumishi waweze kuenea katika vyumba vya kutolea huduma .

Akimkaribisha mkurugenzi, Afisa utumishi Mkuu wa manispaa ya Ilemela Ndugu Egidy Teulas amewapongeza watumishi wa kituo hicho huku akiwaasa kuzingatia taratibu, sheria na kanuni za utumishi wa umma katika uwajibikaji wao .

Mkurugenzi Ummy alitumia nafasi hiyo pia kutembelea mazingira ya kituo hicho pamoja na kukagua utoaji wa huduma kwa wananchi huku akiahidi kuendelea kufanya hivyo katika vituo vyengine vya kutolea huduma za afya .

Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.