• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

MKURUGENZI UMMY AWATAKA WANAMICHEZO WATUMISHI KURUDI NA USHINDI ILEMELA

Posted on: August 30th, 2024

Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela, Bi Ummy Wayayu amewataka wanamichezo watumishi wanaoshiriki mashindano ya michezo ya shirikisho la michezo serikali za mitaa Tanzania (SHIMISEMITA) kuhakikisha wanarudi na ushindi mkubwa Ilemela


Ametoa rai hiyo tarehe 29 Agosti 2024 alipofika kuwajulia hali na watumishi hao yanayoendelea katika  chuo cha ualimu Butimba Mwanza ambapo alitumia fursa hiyo kuwapongeza kwa kuaminika na kuchaguliwa kuiwakilisha Ilemela katika mashindano hayo huku akiwaahidi donge nono pindi watakaporudi na ushindi Ilemela


Nao viongozi wa timu zinazoiwakilisha halmashauri ya manispaa ya Ilemela katika (SHIMISEMITA) kwa niaba ya wanamichezo hao wameahidi kutwaa ubingwa wa mashindano hayo na kurudi na ushindi nyumbani kwa kuzishinda timu zote za maeneo mengine watakazoshindana nazo.


Nahodha wa kikosi cha timu ya mpira wa miguu wanaume cha manispaa ya Ilemela Mwalimu Harith Hamis kutoka shule ya msingi Kilimahewa amesema kuwa timu yake haikuja kushiriki tu mashindano hayo badala yake wamekuja kuchukua ushindi kwani kikosi chao kipo vizuri na kuwataka wapinzani wao kujipanga haswa ili kuikabili timu hiyo vinginevyo watakuwa wamekuja Mwanza kutalii badala ya kushiriki mashindano hayo


Mwalimu Joyce Hepas Mwara  kutoka shule ya msingi Gedeli ni nahodha wa timu ya fani za ndani itakayoshiriki mashindano ya kwaya ambapo amefafanua kuwa ili kauli mbiu ya wilaya hiyo iweze kuwa na maana ya ‘Ilemela ni yetu, tushirikiane kuijenga’ ni lazima wapenzi na mashabiki wajitokeze kwa wingi ili kujionea ubora na ufundi wa kikosi chake kwani wamejipanga kutoa burudani na kurudi na ushindi katika mashindano hayo


Afisa utamaduni kutoka Ilemela Bi Lulu Ndari amesema kuwa timu za wilaya yake zimejiandaa vizuri kwani zilifanya mazoezi ya kutosha na kwamba zinaendelea kushiriki michezo yote ikiwemo mpira wa miguu, mpira wa wavu, mpira wa pete, kuvuta kamba na kwaya huku akiwataka watumishi wa Ilemela kujitokeza kuiunga mkono na kuishabikia ili iweze kupata morali na ari ya kufanya vizuri zaidi wakati wote wa mashindano


Mashindano ya SHIMISEMITA yanaendelea kurindima katika viwanja mbalimbali vya chuo cha ualimu Butimba na Magereza jijini Mwanza yakishirikisha timu zaidi ya 50 kutoka halmashauri za manispaa, halmashauri za wilaya, halmashauri za miji midogo na majiji yakisindikizwa na kauli mbiu isemayo, “Shiriki uchaguzi wa serikali za mitaa kwa maendeleo endelevu”






Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.