• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

MKURUGENZI ILEMELA AWATAKA WANANCHI KUTUMIA GESI BADALA YA MKAA

Posted on: June 5th, 2018

“Tutumie gesi badala ya mkaa,tubadilike na tuache mazoea”Ni kauli yake Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela John Wanga alipomuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongela katika kilele cha maadhimisho ya siku ya mazingira duniani.

Akihutubia wananchi waliofika katika maadhimisho ya siku ya mazingira duniani yaliyoambatana na kauli mbiu isemayo, Mkaa ni gharama, tumia nishati mbadala,  amewaasa wananchi kuacha kukata miti hovyo na kufuata sheria za nchi na kuwataka kufika ofisi ya Mkurugenzi kwa ajili ya kupata kibali pindi wanapotaka kukata miti.

“Unapotaka kukata mti unatakiwa kufika ofisi ya Mkurugenzi kwa ajili ya kupata kibali”, alisema Mkurugenzi.

Aidha amewataka wananchi kutimiza wajibu wao kwa kuhakikisha kuwa wanatunza mazingira kwa kuacha kukata miti hovyo, kuepuka ujenzi holela kwa kufuata sheria za mipangomiji pamoja na kuacha ufugaji holela maeneo ya mjini.

Maadhimisho haya yameenda sambamba na upandaji wa miti ya miembe huku Mkurugenzi akiwataka viongozi wa kata kuhakikisha kuwa miti hiyo inatunzwa ambapo alitoa ufafanuzi kuwa miti iliyopandwa katika maeneo ya watu itunzwe na wahusika wa maeneo hayo na ile iliyopandwa katika maeneo ya wazi ni jukumu lao viongozi kuitunza.

Halikadhalika kupitia kauli mbiu ya siku hii, Mkaa ni gharama, Tumia nishati mbadala amewahimiza wananchi kuzingatia matumizi ya nishati mbadala na suala la usafi wa mazingira.

Nae Diwani wa kata ya Kawekamo ambapo kilele cha maadhimisho ya siku hii yamefanyika, Mhe.Japhes Rwehumbiza ameushukuru mkoa kwa kuhitimishia katika kata yake huku akisisitiza ufikishwaji wa elimu ya matumizi ya nishati mbadala ngazi ya mitaa na kuwa elimu hiyo isiishie katika mabango tu kwani wananchi wengi hawana elimu ya kutosha juu ya nishati mbadala.

“Elimu ya nishati mbadala haijafika kwa wananchi,isiishie kwenye mabango bali ishuke hadi ngazi ya kata”, alisema alipokuwa akimkaribisha mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa Ndugu John Wanga kwa ajili ya kuhitimisha maadhimisho hayo.

Nae Afisa Mazingira wa Manispaa ya Ilemela Ndugu Simon Nzagi amesema kuwa, kauli mbiu hii imekuja kwa muda muafaka na kuwa ina mapana zaidi ya watu wanavyoifikiria na kuwataka wananchi kutumia nishati hizi kwa busara ili kuweza kuhifadhi miti ambapo ikikatwa hovyoo inaweza kusababisha jangwa,ukosefu wa mvua, kupotea kwa wanyama na hatimae kusababisha uchumi wa nchi kushuka.

Ndugu Emmanuel Lufunga ambae ni mmoja wa wananchi waliohudhuria kilele cha maadhimisho hayo ameiomba serikali kuwa maadhimisho haya yasiishie tu mjini bali yafike na vijijini huku akisisitiza utoaji wa elimu ya nishati mbadala.

Kila mwaka ya tarehe 05 mwezi wa sita dunia huadhimisha siku ya mazingira, madhumuni ya maadhimisho ya siku hii ni kutoa fursa ya kukuza uelewa wa jamii kuhusu masuala mbalimbali ya mazingira na kuhamasisha jamii kuchukua hatua za makusudi za kuhifadhi mazingira kwa ustawi wa sasa na maisha ya baadae.



Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.