• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

MKANDARASI AKABIDHIWA ENEO LA KAZI UJENZI WA SOKO LA KIRUMBA NA BARABARA ZINAZOZUNGUKA SOKO

Posted on: November 15th, 2024

Mkandarasi M/S China Railway 15 Bureau Group Cooperation kutoka nchini China atakaetekeleza mradi wa ujenzi wa soko la kirumba na barabara zake zenye urefu wa km 2.9 kwa gharama ya shilingi za kitanzania bilioni 14.71 (bila VAT) amekabidhiwa rasmi eneo la kazi kwa ajili ya kuanza utekelezaji wa mradi huo


Akizungumza wakati wa hafla fupi ya kumkabidhi mkandarasi eneo la kazi iliyofanyika katika viwanja vya ofisi ya kata ya kirumba litakapojengwa soko hilo siku ya tarehe 14 Novemba 2024, mbunge wa jimbo la Ilemela Mhe Dkt Angeline Mabula amemshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuruhusu matumizi ya fedha na kuhakikisha mradi huu unatekelezwa Ilemela, pamoja na hayo amemtaka mkandarasi kutumia wazawa kwa kazi zisizohitaji utaalam mkubwa.

 

“Katika siku niliisubiria kwa hamu ni hii ya leo tunapo mkabidhi mkandarasi eneo kwa ajili ya kazi, maneno yalikuwa mengi lakini leo tunashuhudia kazi inaenda kuanza, tumshukuru sana Rais Dkt Samia”. Alisema Mbunge

 

Aidha Mhe Mabula amewataka wananchi wanaoishi jirani na mradi huo kutanguliza maslahi ya umma mbele kwa kutoa ushirikiano kwa mkandarasi pamoja na kulinda mali na vifaa vyote vitakavyoletwa kwaajili ya ujenzi wa mradi huo ili uweze kukamilika kwa wakati 

 

Kwa upande wake meneja wa wakala wa barabara za mijini na vijijini TARURA mhandisi Sobe Makonyo mbali na kumshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan na serikali yake kwa kutoa fedha za ujenzi wa mradi huo akaongeza kuwa kazi zitakazotekelezwa na mkandarasi ni ujenzi wa soko la kisasa na ujenzi wa barabara zenye urefu wa km 2.9 huku akiahidi kumsimamia mkandarasi ili tija ya mradi huo iweze kufikiwa 

 

Shabani kasiaga ni mwakilishi wa kampuni ya ms china railway 15 bureau group cooperation ambapo ameahidi kufuata miongozo yote iliyopo kwenye mkataba wa ujenzi wa mradi huo huku akiwaomba wananchi na viongozi kutoa ushirikiano wakati wote wa utekelezaji wa mradi huo ili waweze kuukamilisha kwa wakati na ubora unaohitajika

 

Nusura Abdalla Omary na Bakari Said ni wananchi wa kata ya Kirumba na wafanyabiashara wa soko  la zamani katika kata hiyo wao wamepongeza  na kuishukuru serikali kwa hatua iliyofikiwa ya kuhakikisha soko hilo la kisasa linajengwa sambamba na kumtaka mkandaraasi kuhakikisha soko jipya litakapokamilika hakutakuwepo na changamoto ya maji kujaa ndani ya soko kama ilivyokuwa hapo zamani.

Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.