• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

MILIONI 500 KUTOKA MAPATO YA NDANI MANISPAA YA ILEMELA KUJENGA KITUO CHA AFYA

Posted on: July 23rd, 2024

Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela kupitia mapato yake ya ndani imetenga bajeti ya  jumla ya kiasi cha shilingi millioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya ndani ya kata ya Ibungilo mtaa wa Kiloleli A ikiwa ni katika jitihada za kupunguza adha inayowakabili wananchi wa eneo hilo kusafiri umbali mrefu kutafuta huduma za afya.

Akizungumza wakati wa ziara yake ya kukagua shughuli mbalimbali za maendeleo ndani ya kata hiyo mbunge wa jimbo la Ilemela Mhe.Angeline Mabula amesema Manispaa ya Ilemela imeamua kufikia uamuzi wa kubuni miradi mikubwa kwa kutumia fedha za mapato ya ndani kwa kuwa fedha nyingi za mapato ya ndani zimekuwa zikitumika kwa shughuli mbalimbali za kimaendeleo kwa mgawanyo mdogo mdogo.

“ Tumeamua kutenga fedha nyingi za mapato yetu ya Manispaa kwa ajili ya miradi mikubwa ya kuonekana,kata ya Ibungilo ina zaidi ya wakazi 24,000 na haijawahi kuwa na kituo cha afya.Nafikiri ni wakati sasa wa wananchi hawa kusogezewa huduma hizo.”

Aidha Mhe.Mabula ametoa rai kwa wananchi wa kata ya Ibungilo kutoa ushirikiano wa kutosha pindi kazi ya ujenzi itakapoanza na kuwataka kuvaa umiliki wa mali zote zitakazokuwepo kwenye eneo la ujenzi ili kuruhusu kazi iende kwa kasi na mradi kukamilika kwa wakati kwa ajili yao huku akimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kutoa fedha nyingi ndani ya jimbo lake la Ilemela kwa ajili kuchochea shughuli za maendeleo kwa wananchi.

Nae diwani wa kata  hiyo Mhe.Hussein Magela amemshukuru Mbunge wa jimbo la Ilemela kwa kazi nzuri anayoendelea nayo na kuzidi kuahidi ushirikiano mkubwa katika shughuli za kuleta maendeleo ndani ya kata yake.

Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela Silvester Mrimi amepokea maagizo yote ya Mbunge wa Ilemela na kumhakikishia utekelezaji kwa awamu kwa kuangalia uhitaji sambamba na bajeti iliyopangwa katika shughuli za maendeleo.

Mama Doreen ni muuzaji wa ndizi katika soko la Kiloleli ambako Mhe.Mbunge alipita kuwasalimia wafanyabiashara wadogowadogo yeye anampongeza Mhe.Mabula kwa namna anavyotembelea wananchi maeneo mengi kujua changamoto zao na kuzitolea majibu kwa wakati.

“ Anafanya vizuri sana huyu mama,hajatuangusha kina mama wenzie.”  

 Mbali na hayo Mhe.Mabula amekabidhi jumla ya mifuko 100 ya saruji yenye thamani ya shilingi milioni 2.4 kwa ajili ya shughuli za ujenzi na ukarabati wa miradi mbalimbali ya maendeleo ndani ya kata hiyo.

 

Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.