• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

MIKOPO YA ASILIMIA 10 KUINUA UCHUMI WA WANA ILEMELA, BILIONI 1.13 ZATOLEWA

Posted on: March 1st, 2025

Lengo kubwa la serikali ni kuona wananchi wake wanaboresha hali zao za kiuchumi kuanzia ngazi ya familia na taifa kwa ujumla, katika kutekeleza azma hii halmashauri ya manispaa ya Ilemela tarehe 28 Februari 2025 ilitoa mikopo yenye thamani ya shilingi bilioni 1.13 kwa vikundi 60 villivyokidhi vigezo vya wanawake , vijana na watu wenye ulemavu fedha inayotokana na mapato yake ya ndani ya halmashauri.

 

Akikabidhi mfano wa hundi kwa vikundi hivyo katibu tawala wa Wilaya ya Ilemela wakili Mariam Msengi akimwakilisha Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe.Hassan Masala amesema mikopo hiyo ilisimamishwa kutolewa kwa muda kufuatia mapungufu kadhaa yaliyojitokeza kipindi cha nyuma hali iliyopelekea serikali kufanya maboresho katika kuhakikisha wananchi wake wanapata kilicho bora na kwa usalama zaidi hivyo kuwataka wanufaika kwenda kuzitumia kwa malengo yaliyokusudiwa.

 

“Nitoe rai yangu kwenu mtumie fursa hii vizuri , mmepitishwa kwenye madarasa mengi sana hadi kufikia hatua ya kupatiwa mkopo, basi fedha hizi mkazitumie kama ilivyokusudiwa, serikali inatamani kuona fedha hizi zinawainua kiuchumi, fedha hizi zitumike kuboresha hali zetu za kiuchumi, tutakapowatembelea basi tukute mmenyanyuka kiuchumi hilo ndio lengo la kwanza”, alisema wakili Mariam

 

Akiwasilisha taarifa ya utoaji wa mikopo hiyo mkurugenzi wa halmashauri ya manispaa ya Ilemela Bi.Ummy Wayayu amesema kuwa wamezingatia taratibu zote  pamoja muongozo wa utoaji wa mkopo unaozingatia uwiano wa 4:4:2 ambapo vikundi 39 vya wanawake vimeidhinishiwa shilingi milioni 618.60, vikundi 17 vya vijana shilingi milioni 492.90 na vikundi 4 vya watu wenye ulemavu waliidhinishiwa shilingi milioni 24,huku akifafanua kuwa vikundi 32 ambavyo vimekidhi vigezo  vitapewa awamu inayofuata

 

Katika nyakati tofauti wawakilishi wa vikundi vya wanawake, vijana na wenye ulemavu Bi Specioza Alex, Ndg. Jackson Kalunga na Ndg. Yohanna wameishukuru serikali kwa kurejesha utoaji wa mikopo hii ya asilimia 10  na kuahidi  kwenda kuitumia kwa malengo yaliyokusudiwa na kuirejesha kwa wakati ili na vikundi vingine viweze kunufaika, huku wakiahidi kuwa mabalozi wazuri wa serikali yao

Mhe Renatus Mulunga Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilemela ameviasa vikundi hivyo juu ya suala la uadilifu na uaminifu na kusema kuwa baadhi ya vikundi vimekuwa vikitumia fedha hizo kinyume na utaratibu akihitimisha kwa kusema kuwa utoaji wa  mikopo hii utagusa kata zote 19 na utafanyika kwa awamu.

 

 

 

 

 

 

Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • "TUUFANYE USAFI KUWA NI TABIA YA KUDUMUA": ANNA MBAO

    May 31, 2025
  • WATAALAM WA MANISPAA YA ILEMELA WAJENGEWA UWEZO MATUMIZI YA MFUMO WA MANUNUZI WA UMMA

    May 29, 2025
  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.