• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
      • Maadili ya Msingi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • Utumishi na Utawala
        • Mipango na ufuatiliaji
        • Kilimo, Ufugaji na Uvuvi
        • Maendeleo ya Jamii
        • Elimu Sekondari
        • Elimu ya Awali na Msingi
        • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
        • Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe
        • Miundombinu na Uendelezaji wa Miji na Vijiji
      • Vitengo
        • Mazingira na Usafishaji
        • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
        • Michezo, Utamaduni na Sanaa
        • Fedha na Uhasibu
        • Sheria
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Manunuzi
        • TEHAMA na Takwimu
        • Mawasiliano Serikalini
    • Kata
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

MIKOPO YA ASILIMIA 10 INAVYONUFAISHA VIJANA ILEMELA

Posted on: December 16th, 2022

“Ni wakati wa vijana kuamka na kuacha kukaa vijiweni kupoteza muda bila kazi yoyote,zipo fursa nyingi zinazotolewa na Halmashauri ikiwemo mikopo ya asilimia 10 inayojumuisha makundi matatu ambayo ni vijana 4%,wanawake 4% na walemavu 2%.”

Hayo yamesemwa na Afisa uvuvi wa Manispaa ya Ilemela Ivon Maha wakati wa zoezi la uvunaji samaki kwa awamu ya kwanza kwa vikundi vya vijana vya CHAPAKAZI na CATFISH wanaojihusisha na shughuli za uvuvi wa vizimba katika mtaa wa Igalagala ndani ya kata ya Sangabuye.

Maha amesema shughuli hii ya ufugaji wa samaki kwa kutumia vizimba ni mradi wa kiubunifu uliobuniwa na vijana wenyewe na kuungwa mkono na wataalam wa uvuvi wa Manispaa mpaka kufikia hapa huku akiwataka vijana zaidi wajitokeze kufanya kazi za namna hii.

“Vijana mjitokeze kufanya shughuli mbalimbali za uzalishaji nataka niwatie moyo kuwa shughuli za namna za uvuvi zinawezekana mje mpewe mikopo mfanye kazi za namna hii.”Amesema Maha

Aidha Maha amefafanua kuwa vikundi vyote viwili vinafanya kazi katika mtaa wa Igalagala ndani ya kata ya Sangabuye,kila kikundi kina kizimba cha samaki wake ambapo kila kizimba kina takribani ya jumla ya samaki 36,000 ambapo kwa ujumla vikundi hivyo vina jumla ya samaki 72,000.

Nae Afisa vijana wa Manispaa ya Ilemela Bi.Lucy Nicholaus Matemba amesema vikundi hivyo vilipewa jumla ya shilingi za kitanzania 91,880,000 ya asilimia 10 mnamo mwezi Aprili ,2022.

Baraka Buhegu ni mwenyekiti wa kikundi cha CATFISH yeye anatoa shukrani kwa Halmashauri kwa kuwaamini na kutoa kiasi hicho cha fedha kwa wao kufanya ufugaji wa vizimba vya samaki.

“Leo tunavuna samaki 3,000 ambao tunatarajia kuuza shilingi 5,000 kwa kila samaki matarajio yetu ni kupata jumla ya shilingi milioni 15 na baadhi ya wateja tayari tunao.Tunazidi kuwakaribisha kununua samaki wetu wa viwango kwani ndo tumeanza uvunaji.”Amesema Baraka.

 

Announcements

  • MATOKEO KIDATO CHA NNE 2022 SHULE ZA SERIKALI NA BINAFSI MANISPAA YA ILEMELA January 29, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA MAPOKEZI YA FEDHA September 30, 2022
  • TAARIFA YA MAPOKEZI YA FEDHA KATIKA KIPINDI CHA ROBO YA KWANZA JULAI-SEPTEMBA 2022 October 11, 2022
  • MATOKEO YA DARASA LA SABA 2022 December 01, 2022
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • BARAZA LA BIASHARA ILEMELA LAHIMIZA USHIRIKIANO KATI YA SEKTA BINAFSI NA ZA UMMA

    March 18, 2023
  • JAMII YA ILEMELA YATAKIWA KUTUNZA MAZINGIRA

    March 11, 2023
  • WANANCHI ILEMELA WAPONGEZWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO

    March 11, 2023
  • WADAU WA MAENDELEO WAENDELEA KUUNGUA JUHUDI ZA SERIKALI

    March 02, 2023
  • Tazama zaidi

Video

FAHAMU KUHUSU MFUMO WA TAUSI
More Videos

Quick Links

  • Kuhakiki Taarifa za Mpiga Kura
  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip
  • Maombi ya leseni ya biashara

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.