• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

MIAKA 61 YA UHURU MAFANIKIO YA KISEKTA YAONGEZEKA ILEMELA

Posted on: December 10th, 2022

Katika kipindi cha miaka 61 ya uhuru wa Tanganyika tija imeongezeka katika sekta mbalimbali zikiwemo za uzalishaji mali, na huduma za kijamii, utawala bora, ulinzi na usalama kwa ujumla katika kila sekta ndani ya Wilaya ya Ilemela


Hayo yamebainishwa na Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Ndugu Balandya Elikana katika hotuba iliyosomwa na mwakilishi wake Ndugu Emili Kasagara katika kilele cha maadhimisho ya sherehe za miaka 61 ya Uhuru

Kwa upande wa sekta ya viwanda amebainisha kuwa viwanda vingi vinamilikiwa na watanzania wenyewe na hivyo kutoa ajira kwa watanzania na kuongeza kuwa wakati wa utawala wa mkoloni Ilemela hapakuwa na viwanda vikubwa na vya kati ambapo hadi sasa vipo viwanda 12, vya kati 11 na vidogo 286.


Ndugu Kasagara ameongeza kusema kuwa hatua kubwa imepigwa katika sekta ya elimu ambapo hadi sasa zipo shule za msingi na awali 130 tofauti na awali ambapo zilikuwa shule 08 tu za serikali na kwa upande wa elimu sekondari wilaya ina shule 54 za sekondari ambapo shule 32 ni za serikali na shule 22 ni za watu binafsi, mashirika ya dini au taasisi.


Akizungumzia kuhusu suala la Maji Ndugu Kasagara amesema kuwa serikali inatambua changamoto ya maji kwa wananchi hususana Mkoa wa Mwanza na kusema kuwa juhudi zinaendelea kwa kujenga chanzo kikubwa cha maji cha Butimba kinachoenda kutatua tatizo kubwa la maji.


Kuhusu Sekta ya Afya amesema kuwa awali Wilaya haikuwa na kituo chochote cha kutolea hudu,a za afya, lakini kupitia jitihada serikali na wananchi jumla ya vituo vya kutolea huduma za afya vimejengwa ambapo zipo hospitali vinne, vituo vya afya 11 na zahanati 38, kliniki tisa na maternity home (vinne)


Ndugu Kasagara kwa niaba ya Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza amewasisitiza wananchi umuhimu wa kutumia fursa zilizopo za uwekezaji kuondoa umaskini wa kipato na kuboresha hali ya maisha ya wananchi wilaya ya Ilemela kiuchumi na kijamii.


Sherehe hizo za kilele cha maadhimisho ya Miaka 61 ya Uhuru zilitoa fursa ya kongamano ambapo mada kubwa iliyojadiliwa ikiwa ni “ Maendeleo ya Tanzania baada ya Uhuru” ambapo mada mbalimbali juu ya elimu, afya, miundombinu, teknolojia na maendeleo ya kiuchumi ziliwasilishwa.



“Amani na Umoja ni Nguzo ya Maendeleo Yetu”, ni kauli ya mbiu ya miaka 61 ya Uhuru ambapo wananchi wametakiwa kuiishi kwa vitendo kwa kuhakikisha wanalinda na kudumisha Amani na Umoja kwani ndio tunu ya Taifa la Tanzania.

Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.