• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Mhe. Masala asisitiza uadilifu katika mradi wa ujenzi kituo cha afya Kayenze

Posted on: October 12th, 2021

Mhe Hasan Masala, Mkuu wa Wilaya ya Ilemela amesisitiza suala la uadilifu katika mradi wa ujenzi wa kituo cha afya cha Kayenze. Hayo ameyasema wakati wa kuchimba msingi wa kituo hicho ikiwa ni ishara ya kuzindua rasmi ujenzi wa kituo cha afya cha Kayenze.

“Nisistize kama kiongozi wa serikali, uadilifu katika utekelezaji wa mradi huu, kwani fedha hii inatazamwa na wengi, mtu asijaribu kupata kishawishi atakaejaribu kufanya yale ambayo yapo nje ya muongozo wa fedha hii atapata changamoto”.

Aidha Mhe. Masala amezitaka Kamati zikawajibike, kwa kuhakikisha kuwa kumbukumbu zinatunzwa vizuri kuanzia shilingi ya kwanza hadi itapoishia kwani lengo ni kupata zaidi ya majengo matatu na kumaliza mradi kwa ukamilifu wake na ikiwezekana kujenga majengo ya ziada.

Pamoja na maelekezo hayo amewapongeza wananchi kwa utayari wao kuupokea mradi huu, kutoa eneo la ujenzi, na kusema kuwa  viongozi watahakikisha kuwa fedha hizi hazitakaa kwenye akaunti na zitafanya kazi iliyokusudiwa ili wananchi waweze kupata majibu ya kero walizokuwa nazo. Huku akiwataka wananchi kumshukuru Mhe. Rais kwa kuleta kiasi cha shilingi 250 kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya Kayenze.

Nae Diwani wa Kata ya Kayenze,Mhe. Issa Dida amemshukuru Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuleta fedha za ujenzi wa kituo cha Afya katika kata yake kwani kero ya umbali wa kufuata huduma za afya inaenda kutatuliwa sasa.

Malengo ya ilani ya chama cha mapinduzi ni kutaka kila mwananchi kuwa na  afya bora, nguvu ili kuweze kushiriki katika shughuli za ujenzi wa taifa lakini pia kuleta maendeleo katika familia zao. Huku akichambua kwa ufupi Ilani ya CCM upande wa afya kwa kusema kuwa, maandiko ya CCM kwenye ilani ya uchaguzi yanasema kuwa kila palipo na mtaa pawe na zahanati, palipo na kata kuwe na kituo cha afya, na palipo na wilaya iwepo hospitali ya wilaya hayo yamesemwa na katibu wa CCM wa wilaya ya Ilemela  Bi Aziza Isimbula.

Nae Mbunge wa jimbo la Ilemela, Mhe. Angeline Mabula ambae alishiriki zoezi hilo la uchimbaji wa msingi, amewaomba wananchi wa kata ya kayenze kuilipa heshima ya kupewa kituo cha afya kayenze kwa kufanya kazi ya mfano na ya viwango isiyokuwa na udokozi huku akitaka kila mtu kuwa mlinzi wa  mwenzake,

“Mhe Rais mmemsikia, kuwa ukitaka kumjua rangi zake mchezee pesa, tunachotaka ujenzi wa viwango tushirikiane na kuhakikisha kuwa kazi hii inaenda vizuri”,Alisisitiza

Katika zoezi hilo, Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela Mhandisi Modest Apolinary amesema kuwa anatarajia kuwa kazi itaanza mara moja, huku akiwahimiza wakazi wa Kayenze kujitolea kufanya kazi kwani kazi watakayofanya kwa nguvu zao itasaidia kuokoa fedha nyingi, na kuahidi  kuchangia matofali elfu kumi katika ujenzi huo.

“Hii kazi ni yenu mjitahidi kutoa nguvu zenu kuchangia ili fedha itakayo okolewa isaidie kujenga jengo jingine”,Alisema.

Halmashauri   ya   Manispaa   ya   Ilemela   ilipokea   fedha   kiasi   cha Shilingi Milioni mia mbili na hamsini kutoka Serikali Kuu kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha hicho afya ambapo yatajengwa majengo ya awali ambayo ni jengo la wagonjwa wa nje (OPD),jengo   la   maabara   na   kichomea   taka.

Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.