• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

MHE MASALA AMEWATAKA WALIMU ILEMELA KUSIMAMIA NIDHAMU SHULENI

Posted on: May 29th, 2024

Walimu wa shule za msingi na sekondari katika halmashauri ya manispaa ya Ilemela wametakiwa kuhakikisha wanasimamia nidhamu na maadili ya wanafunzi sambamba na kuzidisha bidii katika ufundishaji.


Kauli hiyo imetolewa na Mhe Hassan Masala Mkuu wa Wilaya ya Ilemela katika kikao kilichowakutanisha wadau wa elimu kwa lengo la kutathmini hali ya elimu wilayani Ilemela.


“Tusimamie nidhamu ya watoto wetu, ni wajibu wetu tutimize hilo, tujitahidi kulinda usalama wa watoto wetu kesi za ulawiti zimekuwa nyingi sana hivyo watoto wetu hawapo salama sana, tunalo jukumu la kuweka mkakati wa pamoja wa kuwalinda watoto ikiwa ni pamoja na kuzikagua shule zetu” amesisitiza Mhe Masala


Mhe Masala ameendelea kusisitiza kwa kuwataka walimu kuongeza bidii katika ufundishaji, kwani ni matamanio yake kuona Ilemela inashika nafasi ya kwanza kimkoa,  amesisitiza


Aidha ili kuweza kutatua changamoto ya upungufu wa vyumba vya madarasa kutokana na kuwa na idadi kubwa ya wanafunzi katika shule, Mhe Masala amewataka waheshimiwa madiwani kuwahamasisha wananchi juu ya ujenzi wa madarasa mapya.


“Kuna madarasa lazima tuyaongeze nikuombe Mstahiki Meya kwenye vikao vyenu muweke mkakati wa kuona namna ambavyo tutajenga madarasa mapya kwani  tunao upungufu wa vyumba vya madarasa 193. Ni matarajio na matamanio yetu kuona tunazimaliza hizi changamoto, na yote yanawezekana kama dhamira yetu tunaiweka inakuwa ni kitu kimoja”, Amesema Mhe Masala


Akichangia katika kikao hicho Mwenyekiti wa kamati ya huduma za jamii na diwani wa kata ya Ibungilo Mhe Hussein Magera ameomba nguvu zaidi ielekezwe sekta ya elimu msingi kwani bado changamoto ni kubwa ya upungufu wa madarasa na madawati huku akishauri juu ya kubadili mfumo wa ujenzi wa madarasa kutoka madarasa ya kusambaa na kujenga mfumo wa ghorofa ili kuweza kuhifadhi maeneo katika shule zetu.  


Ummy Wayayu ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela nae amewahimiza walimu kuhakikisha watoto wanafundishwa stadi za maisha kuanzia wakiwa na umri mdogo ili watakapokuwa watu wazima wakayaishi mafundisho hayo


“Unapomfundisha mtoto akiwa mdogo ataenda kuyaishi maisha hayo akiwa mkubwa hivyo walimu tunaokaa na hawa watoto tuangalie namna ya kuwakuza katika njia bora”


Bi Sitta Kirawe ni Mkuu wa shule ya sekondari Nundu na Bwana Nashir Wamuraza mwalimu mkuu shule ya msingi Buzuruga D wamemshukuru Mkuu wa Wilaya kwa kikao chenye tija katika kuboresha elimu Ilemela na kuahidi kwenda kutekeleza yale waliyoelekezwa kwa kushirikiana na wadau wengine kwenye kata wakitolea mfano juu ya ya namna watakavyodhibiti suala la utoro wa walimu na watoto kwa kushirikisha wazazi na kamati za shule ikiwa na pamoja na kushirikisha uongozi wa kata


Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.