• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

MHE MASALA AKABIDHI OFISI, AWASHUKURU WATUMISHI WA ILEMELA KWA USHIRIKIANO

Posted on: July 14th, 2025

"Nimefanya kazi hapa miaka 4 kwa mara ya kwanza niliteuliwa tarehe 21 Juni 2021 na kwa muda niliokaa hapa ninayo mengi ya kusimulia, mengi ya kuyasema na mengi ya kushuhudia, itoshe kuwashukuru wote tuliofanya kazi kama timu moja kwa ajili ya kusukuma gurudumu la maendeleo la wilaya ya Ilemela na mkoa wa mwanza kwa ujumla"

 

Ni kauli ya Mhe Hassan Elias Masala aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Ilemela wakati akimkabidhi ofisi rasmi Mkuu mpya wa Wilaya ya Ilemela Mhe Amir Mohamed Mkalipa, siku ya Jumatatu tarehe 14 Julai 2025, huku akiwataka watumishi kuendeleza ushirikiano waliokuwa wakimpatia wakati wa uongozi wake akiwa wilayani hapa.

 

Sambamba na hilo ameishukuru Kamati ya Usalama ya Wilaya, Kamati ya siasa ya Wilaya, Mbunge wa jimbo na Mkurugenzi na timu yake ya watumishi kwa ushirikiano wao waliompatia katika kutekeleza majukumu yake ya kila siku.

 

Nae Mhe Amir Mkalipa Mkuu wa Wilaya ya Ilemela akiongea na hadhira iliyoshuhudia makabidhiano hayo amemshukuru Mhe Masala pamoja na kuwaomba ushirikiano watendaji wote wa Ilemela kwa kufanya kazi pamoja ili kuweza kumsaidia Mhe Rais.

 

"Neno ninalolichukua kutoka kwa Mhe Hassan Masala, ni kwamba hawa wamefanya kazi yangu kuwa rahisi, niwaombe muendelee kuifanya kazi yangu kuwa rahisi, tukafanye kazi pamoja ya kumsaidia Rais Dkt Samia"

 

Bi Ummy Wayayu Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela amemshukuru Mhe Masala kwa ushirikiano wake katika kipindi ambacho wamefanya nae kazi kwa takriban mwaka mmoja.Huku akimkaribisha Mhe Mkalipa na kumuahidi ushirikiano wa kutosha 

 

"Nikushukuru kiongozi tumefanya kazi nzuri sana kwa karibu na kwa ushirikiano mkubwa,kwako Mhe mkalipa nikukaribishe Ilemela, tuna imani pale alipoachia Mhe Masala basi utashika kijiti kwenda mbele zaidi ya pale alipoishia yeye nikiwa na imani kubwa kuwa kupitia uongozi wako tutakwenda vizuri zaidi", amesema Bi Ummy

 

Hassan Millanga ambae ni katibu wa CCM Wilaya ya Ilemela, akimuelezea Mhe Masala amesema kuwa  Mhe Masala ni kiongozi mshirikishaji siku zote madirisha yake yalikuwa wazi  kwa chama ambapo akatumia wasaa huo kumshukuru Mungu kwa kumpata mtu mwema, mambo ambayo huwa hayatokei mara kwa mara na kumuahidi Mhe Mkalipa kumpa ushirikiano wa kutosha. 

 

Takribani wiki tatu zimepita toka Mhe Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alipofanya mabadiliko na uteuzi wa viongozi mbalimbali, na Wilaya ya Ilemela ni miongoni mwa wilaya zilizoguswa na mabadiliko hayo.

 

Announcements

  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2025 July 08, 2025
  • TANGAZO LA KAZI NAFASI YA UDEREVA DARAJA LA II June 04, 2025
  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • MHE MASALA AKABIDHI OFISI, AWASHUKURU WATUMISHI WA ILEMELA KWA USHIRIKIANO

    July 14, 2025
  • CHANJO YA KUKU KUWANUFAISHA WAFUGAJI

    July 09, 2025
  • PROF NAGU AMEWATAKA WATUMISHI KADA YA AFYA KUENDELEA KUTOA HUDUMA BORA KWA WANANCHI

    July 08, 2025
  • WALIMU WA AJIRA MPYA WAMETAKIWA KUWEKA MIPANGO SAHIHI YA KAZI

    July 04, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.