Mbunge wa jimbo la Ilemela,na Waziri wa Ardhi Nyumba na maendeleo ya Makazi Mhe Dkt. Angeline Mabula amewahimiza wananchi wa Ilemela kuhakikisha wanaendelea kushirikiana na serikali katika kuyafikia maendeleo.
Ameyasema hayo wakati wa ziara ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa kupitia fedha za Serikali kuu, mfuko wa jimbo, mapato ya ndani na fedha za wananchi.
"Maendeleo hayawezi kufikiwa kama hakuna ushirikiano, na kadri tunavyoendelea kuibua miradi na Serikali inapata nguvu ya kuweka mkono wake"amesema Mhe Mabula.
Sambamba na rai hiyo amewapongeza Wananchi wanavyoshirikiana na madiwani kuibua miradi mbalimbali ya maendeleo katika kata zao huku akielekeza kuhakikisha kuwa taarifa za mapato na matumizi zinasomwa katika mikutano ya hadhara ili wananchi waendelee kuguswa kuchangia maendeleo.
Aidha amemuelekeza Afisa Ardhi wa Manispaa kuhakikisha kila taasisi inakuwa na hati miliki ili kuepusha migogoro ya ardhi.
Nao Madiwani kutoka kata za Mecco, Ibungilo, Nyamanoro, Pasiansi na Kitangiri wamemshukuru Mhe Mabula kwa namna ambavyo amekuwa nao bega kwa bega katika maendeleo ya kata zao kwa kutoa matofali na hata kutetea Manispaa ya Ilemela kupata fedha za utekelezaji wa miradi mbalimbali.
Laban ambae ni mwanafunzi wa chuo cha mipango ameishukuru serikali kwa jitihada zake katika kuwaletea wananchi maendeleo akitoa rai kwa wananchi wengine kujitokeza kuunga juhudi za serikali, ameyasema hayo wakati Mbunge alipokagua maendeleo ya ujenzi wa Zahanati mtaa wa Bwiru Press
Katibu Tawala wa Wilaya ya Ilemela , Wakili Mariam Msengi akimwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Ilemela amempongeza Mbunge kwa jitihada zake huku akiahidi kuendelea kuunga mkono jitihada zote za kuwaletea wananchi maendeleo.
Katika ziara hiyo Mbunge aliweka jiwe la Msingi ofisi ya Kata ya Mecco na kukagua ujenzi wa vyumba vya madarasa katika kata ya ibungilo, ujenzi wa zahanati za Kitangiri na Pasiansi na ujenzi wa ofisi ya mtaa wa Kilimahewa A kata ya Nyamanoro.
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
Postal Address: 735 MWANZA
Telephone: + 255 736 200910
Mobile:
Email: md@ilemelamc.go.tz
Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.