• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

MHE JENISTA MHAGAMA:, "MIRADI HII YA TASAF IKAMILIKE KWANI FEDHA ZIPO"

Posted on: February 20th, 2023

Mhe Jenista Mhagama (Mb), Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora ametoa maelekezo kwa uongozi wa Ilemela kuhakikisha kuwa miradi yote ya TASAF inakamilika.


Ameyasema hayo wakati wa ziara ya kikazi aliyofanya akikagua utekelezaji wa miradi ya TASAF III katika wilaya ya Ilemela, ambapo amekagua mradi wa ujenzi wa zahanati ya mihama pamoja na nyumba ya mtumishi.

“Miradi hii ikamilike haraka sana kwani mifumo imefunguka, fedha zipo na wananchi wapo, na miradi hii kumi itakapokamilika , naomba kuahidi kuwa tutaleta miradi mingine kumi kupitia fedha hizi za OPEC chini ya TASAF” ,Mhe Mhagama


Mhe Mhagama ameongeza kusema kuwa itakapofika mwezi wa nne ni lazima turudi hapa tuanze kuona zahanati hii inaanza kazi hatuna haja ya kuchelewesha miradi hii mikubwa hasa hii inayojibu kero na mahitaji makubwa ya wananchi wetu na hasa akina mama, watoto na wazee hivyo tuna kila sababu ya kuhakikisha kuwa miradi hii inakamilika mapema.

Kuhusu malalamiko juu ya walengwa wa TASAF wasiokuwa na sifa, amewaeleza walengwa hao kuwa jambo hilo la mtu ambae hana sifa lipo mikononi mwao, utaratibu wa kumchagua mwenye sifa unafanyika kwenye mitaa yao, pamoja na hayo akatoa maelekezo kwa uongozi wa Ilemela kuanza kufanya mikutano katika mitaa kwa ajili ya kufanya tathmini ya walengwa wa TASAF.


“Fedha hizi anatakiwa apate mlengwa ambae anazingatia vigezo, na kila mtu akimuona aone kuwa anastahili kutunzwa na mfuko wa TASAF hivyo nikuombe Mhe. DC usimamie swala hili”, Mhe Mhagama


Naye, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima amemhakikishia Waziri Mhagama kukamilisha Ujenzi wa Zahanati na Nyumba ya mtumishi kwenye mtaa wa Mihama ili wananchi waanze kupata huduma za afya kufikia Machi 28, 2023 hasa kwa huduma za afya ya Mama na Mtoto na Lishe.


Vilevile, Mhe. Hassan Masala, Mkuu wa Wilaya ya Ilemela ametumia wasaa huo kumshukuru Mhe. Rais kwa kuwaletea Miradi ya TASAF wananchi wa Kata ya Kitangiri huku akibainisha kuwa imeendelea kuleta chachu kwenye maendeleo na amewapongeza wanannchi wa kata hiyo hasa wa Mitaa ya Jiwe Kuu na Mihama kwani awali wananchi walikua na kiu ya kupata zahanati kwenye eneo lao.

Akishukuru kwa niaba ya wananchi wa Kitangiri hususan mitaa ya mihama na jiwe kuu , Diwani wa kata ya Kitangiri Mhe. Donald Protas, amesema kuwa TASAF imeweka historia kwenye kata yao kwani imesababisha kuanza kwa maendeleo ya kasi  katika sekta ya afya , huku akiwashukuru na kuwapongeza wananchi wa mitaa hiyo kwa namna ambavyo wamejitolea kuhakikisha zahanati hiyo inajengwa .



Leonard Robert mratibu wa TASAF ilemela, katika taarifa yake amesema kuwa kukamilika kwa mradi huu ambao unatarajiwa kugharimu takriban kiasi cha shilingi milioni 219. 25, kutasaidia kusogeza huduma ya afya ya uzazi, maendeleo ya mtoto na lishe karibu zaidi na wananchi.

Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.