• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

MHANDISI KUNDO ALETA MATUMAINI SEKTA YA MAJI ILEMELA

Posted on: July 26th, 2024


Naibu Waziri wa maji Mhandisi Kundo Mathew ameleta matumaini ya upatikanaji wa maji katika maeneo yote ya Wilaya ya Ilemela.

Akizungumza wakati wa mkutano wa hadhara kusikiliza kero za maji uliofanyika viwanja vya shule ya msingi Buswelu Mhe . Kundo amesema upatikanaji wa huduma ya maji kwa wananchi ni moja ya kipaumbele cha serikali ya awamu ya sita.

" Upatikanaji wa maji safi na salama ni kipaumbele chetu kwa kuanzia maeneo yote ya umma. Mhe. Rais anataka wananchi wake wote wapate maji na mimi sitakubali kumkwamisha . "

Ameitaka mamlaka ya maji Mwanza ( MWAUWASA ) kuhakikisha maji yanapatikana maeneo yote yenye miundo mbinu rafiki na kuwataka wataalam wake kuendelea kusambaza na kufukia mabomba kwa wakati ili kuepuka uharibifu wake.

Akijibu hoja ya Dominic Thomas mkazi wa mtaa wa Nyamadoke kata ya Nyamhongolo kuhusu suala la wananchi kununua vifaa vya kuunganishia maji MWAUWASA tu na si sehemu nyingine Mhe. Kundo ametoa maelekezo kwa wananchi kupata muongozo wa aina "specification"  ya vifaa vya ubora unaohitajika kutoka kwa wataalam wa MWAUWASA na kununua vifaa hivyo popote huku akiwasihi kuacha kazi ya kufunga vifaa hivyo iwe ya mafundi wataalam kutoka MWAUWASA.

" Wananchi ombeni kuunganishiwa maji kwa maandishi,kazi ya kuunganisha ni ya fundi na nyinyi msiwe mafundi muache fundi afanye kazi yake akiharibu tupate wa kumuwajibisha."

Aidha amewataka wananchi kutunza , kulinda mita na miundo mbinu yote ya maji huku akiwasihi MWAUWASA kuanza kutoa elimu juu ya umuhimu wa kuwa na miundo mbinu kuanzia kwenye vyanzo vya maji hadi kumfikia mtumiaji.

Nae Kaimu Mkurugenzi wa MWAUWASA Bi. Nelly Msuya amesema zaidi ya wananchi 340 wa Ilemela wameunganishiwa huduma hiyo na kukiri kusimama kwa zoezi hilo kutokana na kuisha kwa vifaa  vya kuunganishia huku akiahidi vifaa kupatikana mwezi Agosti 2024 na zoezi kuendelea mara moja.

Mhe. Sarah Ng'hwani ni diwani wa kata ya Buswelu anamshukuru Mbunge wa Ilemela Mhe.Dkt. Angeline Mabula kwa kupokea kero mbalimbali na kuzifikisha bungeni ambako zinafanyiwa kazi kwa wakati.

Akihitimisha mkutano huo Mhe. Mabula ameunga mkono juhudi za kumtua mama ndoo kichwani huku akimshukuru Rais Samia kwa kuendelea kutoa fedha nyingi jimboni mwake kwa ajili ya miradi mbalimbali ya maendeleo.

Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.