• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Mgogoro wa ardhi Kigoto wahitimishwa rasmi

Posted on: March 4th, 2021

Mgogoro wa ardhi katika eneo la Kigoto kata ya Kirumba uliodumu muda mrefu kwa zaidi ya miaka thelathini iliyopita umehitimishwa rasmi na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya makazi Mhe. William Lukuvi alipogawa ankara za malipo kwa wananchi wa eneo hilo la Kigoto.


Waziri Lukuvi akihutubia wananchi wa kigoto amesema kuwa amekuja kuhitimisha mgogoro huo rasmi kwa kuwakabidhi wananchi hao ankara za malipo ili waweze kuandaliwa hati ya miaka 99 na hii ikiwa ni baada ya uamuzi wa Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuagiza kuwa wananchi hao wamilikshwe ardhi.

Aliongeza kwa kusema kuwa jumla ekari 56 za serikali zimetolewa kwa wananchi wa eneo la Kigoto huku jumla ya ekari 16 zikiwa zimebaki katika Jeshi la polisi kwa kufuata maelekezo ya Mhe. Rais.


Akigawa ankara hizo za viwanja 600 kwa wananchi wa Kigoto, ameitaka Idara ya ardhi kuhakikisha kuwa mwananchi anapolipia gharama za umilikishaji anapatiwa hati yake ndani ya siku 7.

Aidha amewahimiza wananchi kuhakikisha wanafanya malipo yaliyoainishwa katika ankara za malipo ili waweze kupatiwa hati na amesema kuwa angefurahi iwapo wananchi wote ndani ya miezi 3 wawe wamelipia na kumiliki hati zao ili ziweze kuwasaidia kujikwamua kiuchumi.


Akifikisha salam za Mhe. Rais na kusema kuwa, Rais Magufuli amewataka wananchi wa eneo hilo kuondoa hofu kwani eneo hilo la serikali la ukubwa wa ekari 56 limetolewa bure kwa wananchi, na gharama zitakuwa ni kwa ajili ya kulipia umilikishwaji tu na si vinginevyo.


Pamoja na hayo Waziri Lukuvi amewataka wananchi kuacha kuvamia maeneo ya serikali kwa  kudhani kuwa watakuja kumilikishwa na kuzitaka taasisi zote za serikali kuhakikisha wayalinda maeneo yao yasivamiwe kwani ni jukumu lao.


Nae Mbunge wa Jimbo la Ilemela, Mhe Angeline Mabula amemshukuru Mhe. Rais kwa kutatua mgogoro huu uliokuwa ukileta adha kubwa kwa wananchi kwani wananchi walishindwa kupata huduma mbalimbali za kijamii


Kupitia wananchi wa Kigoto Mhe Mbunge amewaahidi wananchi wa Ilemela kuwa atahakikisha changamoto za migogoro ya ardhi zinatatuliwa na kuisha kabisa.


Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, amemshukuru Rais kwa kitendo chake cha kuwajali wanyonge na kusema kuwa kitendo cha kuwapa bure wananchi ekari 56 inaonyesha ni namna gani Rais anawajali wananchi wanyonge.


“Ekari 16 zimebaki kwa jeshi la polisi huku ekari 56 zikienda kwa wananchi, hali hii inadhihirisha kuwa Mhe. Rais anatetea wananchi wanyonge”, Alisema.


Mgogoro huu uliohusisha jeshi la polisi na wananchi ulianza kutatuliwa na serikali kuanzia mwaka 2017 ambapo ulipitia katika hatua mbalimbali chini ya Wizara ya ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi.





Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.