• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Mganga Mkuu Ilemela awataka wadau kuendelea kuunga mkono jithada za serikali

Posted on: April 15th, 2021

Ndugu Charles Marwa ambaye ni Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela amewataka wadau mbalimbali kujitokeza na kuendelea kuunga mkono jitihada zinazochukuliwa na Serikali katika shughuli za kimaendeleo hata bila ya kuombwa.

Rai hiyo ameitoa alipokuwa akipokea vifaa mbalimbali vilivyotolewa na  Shirika lisilo la kiserikali la SOS Children’s Village Tanzania linalojishughulisha na malezi ya watoto kwa ajili ya kuimarisha sekta za Afya na Elimu katika Manispaa ya Ilemela.


Nae Mama Doroth Ndege ambae ni Meneja mradi wa shirika hilo Mkoani Mwanza amesema kuwa jumla ya shilingi Milioni 50,875,500 imetumika katika manunuzi ya vifaa hivyo vinavyotarajiwa kunufaisha wananchi wapatao 472,800 wanaopatiwa huduma ya afya katika vituo vya kutolea huduma ya afya  huku upatikanaji wa vitabu vya ziada na kiada kunufaisha wanafunzi  1093 ndani ya Manispaa ya Ilemela.


Mkurugenzi wa shirika la SOS Children’s village Tanzania ndugu David Mlongo amesema shirika lake litaendelea kuunga mkono jitihada za serikali za kuleta maendeleo maeneo yote ambako shirika linafanya kazi zake nchini.


“SOS Children’s village Tanzania ni shirika linalojali maendeleo kuanzia ngazi ya familia kupitia malezi ya watoto, na ni wadau wakubwa wa maendeleo katika mkoa huu wa Mwanza, tunashukuru kwa kupokelewa vizuri katika wilaya hii ya Ilemela na shughuli zetu zimekuwa za kuzaa matunda tunayoyakusudia hivyo nasi hatuna budi kurudisha katika jamii ndio maana leo hii tumeamua kuunga mkono juhudi za maendeleo katika Manispaa ya Ilemela”. Alisema


Aidha Mkurugenzi Mlongo mbali na kuelezea fursa mbalimbali zinazotolewa na shirika lake ikiwemo kutoa elimu na kuziwezesha familia kiuchumi ili walezi waweze kutoa huduma ipasavyo kwa watoto walio katika mazingira magumu pamoja na vijana waweze kufikia ndoto zao akatumia fursa hiyo kuwataka wananchi na wadau wengine kuendelea kuungana pamoja ili kupambana na maadui wakuu wa tatu wa tangu kipindi cha uhuru kwa maana ya ujinga, umasikini na maradhi.


Mganga Mkuu kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela amemshukuru Mkurugenzi wa SOS na kuupongeza uongozi mzima wa shirika hilo kwa jitihada zao za kuhamasisha wadau mbalimbali wa maendeleo  ikiwemo asasi zisizo za kiserikali huku akiahidi kutumia vizuri vifaa vyote vilivyotolewa ili vikatekeleze lengo lililokusudiwa


Vifaa vilivyotolewa ni pamoja dawa za kuongeza damu( Fefo 200mg) boksi 990,gloves boksi 250,gauze absorbent rola 100,vifaa mbalimbali vya steshenari kama karatasi za kuandikia “ream paper”,mashine ya kutolea kopi pamoja na vitabu vya ziada na kiada ambapo vitabu vya shule ya msingi  pisi 551 vimetolewa na vya sekondari pisi 574.





Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.