• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

VIKUNDI 77 VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU VYAPATIWA MAFUNZO

Posted on: March 25th, 2020

Katika kutekeleza agizo la serikali kwa kila Halmashauri la kutoa asilimia 10 ya mapato yake ya ndani kwa ajili ya kuwakopesha vikundi vya wanawake asilimia 4,vijana asilimia 4 na watu wenye ulemavu asilimia 2, Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela kupitia Idara ya Maendeleo ya jamii imeendesha mafunzo ya mikopo kwa vikundi ambavyo vitapatiwa mkopo.

Mafunzo hayo yametolewa kwa awamu na wataalam wa maendeleo ya jamii kwa vikundi takribani 70 lengo ikiwa ni kuwakumbusha malengo ya serikali katika utoaji wa mikopo bila riba ,kufundishwa kanuni na sheria mbalimbali juu ya mikopo sambamba na elimu ya ujazaji wa mikataba .


Wakati wa mafunzo hayo Mkuu wa idara ya Maendeleo ya jamii Ndugu Sitta Singibala ametoa rai kwa vikundi vyote vinavyopata mikopo kutumia kwa malengo ili waweze kurejesha kwa wakati kuepuka usumbufu wa kudaiwa kwa nguvu hadi kwenye vyombo vya sheria, kitu kinachopoteza muda wa kuzalisha na kuminya fursa za wanajamii wengine kupata mkopo.


“Ni muhimu fedha ziwekwe kwenye mzunguko wa biashara au shughuli ya kuzalisha yenye kuingiza fedha ili kurahisisha zoezi la urejeshaji fedha za mkopo”alisema Sitta Singibala.


Aidha Afisa Maendeleo msaidizi Bi.Florence Vedasto amesisititiza wanavikundi kufata taratibu za kifedha katika kurejesha mikopo yao. “Kufata taratibu za kurejesha mikopo ni lazima kwani zoezi linakuwa katika mfumo mzuri na wa kueleweka.Akaunti ya kutumia ni 0150478109500 ya benki ya CRDB.Mkumbuke baada ya kupata slipu ya benki mnaileta Manispaa ili kupata risiti nyingine ya kuthibitisha marejesho yako yamepokelewa.”


Akiongezea wakati wa mafunzo hayo Afisa maendeleo ya jamii Bi.Amina Bululu amesema ni lazima vikundi kufanya kazi kwa malengo na bidii ili tija ya watu kuwa pamoja ionekane.


“Ni wakati wa vikundi kufanya kazi kama kikundi kweli na sio maigizo.Ni muhimu kuwa na miradi ya pamoja ili kupata matokeo makubwa na ya pamoja katika kuleta maana halisi ya vikundi.”


Akihitimisha mafunzo hayo Afisa vijana wa Manispaa ya Ilemela Bi.Lucy Matemba amewataka wanavikundi hao hasahas vikundi vya vijana kuzingatia umri wao.Umri wa kijana ni kuanzia miaka 18 hadi 35 kwa mujibu sheria ya Tanzania


“Ukiona umri wako umezidi jitoe au omba kuwa mlezi wa kikundi ili wengine wenye umri husika wapate nafasi ya kujiunga.Tunataka mikopo hii izae matunda chanya ya kusika Tanzania nzima,msisite kuuliza kwetu mnapokwama.Tupo kwa ajili yenu”


Manispaa ya Ilemela inatarajia kutoa jumla ya shilingi Milioni 197 kwa vikundi 77 vinavyojumuisha vikundi vya wanawake 59, vijana 15 na vikundi vya watu wenye ulemavu vitatu ndani ya Wilaya ya Ilemela kwa kipindi cha kuanzia mwezi Januari hadi machi 2020


Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.