• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

"MAENDELEO ENDELEVU YANATOKA NA SISI WENYEWE"- MHE DKT ANGELINE MABULA

Posted on: August 6th, 2022

Na Violencea Mbakile- IlemelaMc


“Maendeleo endelevu yanatokana na sisi wenyewe kumiliki miradi tunayoletewa na ile ambayo tumeshiriki bila ushiriki wetu hatuwezi kuona nini kinaendelea kwa hiyo hiki tulichokifanya hapa iwe ni muendelezo katika miradi yetu”,Mhe Dkt. Mabula


Mhe. Dkt Angeline Mabula, ambae ni Mbunge wa jimbo la Ilemela na Waziri wa Ardhi, Nyumba na maendeleo ya makazi ameyasema hayo wakati akihutubia wananchi wa Ilemela mara baada ya uzinduzi wa majengo mawili ya mama na mtoto katika zahanati za Ilemela na Nyakato pamoja na uwekaji wa jiwe la msingi katika jengo la wodi ya wazazi lililopo kituo cha Afya Buzuruga.



“Sidhani kama mtakubali mtu achezee miundombinu hii kwani nguvu yako iko hapo na hii ndio maana halisi ya maendeleo endelevu yanayotokana na sisi wenyewe kumiliki miradi tunayoletewa na ile ambayo tumeshiriki” Amesema Mhe Mabula


Pamoja na hayo amewapongeza wananchi wa Ilemela kwa namna ambayo wamekuwa wakishiriki katika miradi mbalimbali ya maendeleo huku akitolea mfano namna ambavyo wananchi wa kata ya Nyakato wameweza kuchangia kiasi cha Tshs. Milioni 10.4 katika ujenzi wa jengo la mama na mtoto katika zahanati ya Nyakato na kusema kuwa kazi kubwa imefanyika.


“Nawapongeza sana wananchi, milioni 10.4 kutoka kwa wananchi ni kazi kubwa imefanyika na haya ndio Mhe Rais anayataka, hataki maneno maneno anataka kazi ifanyike hapo kuna mkono wa wananchi, mbunge na serikali tunapounganisha nguvu siku zote mambo lazima yaende mbele na unapotaka kupika ili chakula kiive lazima uwe na mafiga matatu katika maendeleo na katika majengo ya mama na mtoto haya hapa tumeenda na mafiga matatu yaani wananchi, Mbunge na Halmashauri” amesema akiwapongeza wananchi

Mhe. Dkt Angeline Mabula ametumia hadhara hiyo kumpngeza Mkuu wa Wilaya ya Ilemela kwa ubunifu wake ambao umeongeza kasi ya maendeleo katika sekta zote na kusisitiza kuendelea na umoja huu kwa kuwashirikisha wananchi kwani wameshafahamu elimu ya kujitegemea na kwasababu wanajua kuwa Mhe.Rais yupo tayari kuhakikisha kwamba nguvu ya wananchi haipotei.



“Mhe.Mkuu wa Wilaya sina shaka na wewe na timu yako na tuendelee na umoja huu tukiwashirikisha wananchi wetu kinachonifurahisha ni ushiriki wa wananchi kwa sababu wamefahamu elimu ya kujitegemea na kwasababu wanajua kuwa Mhe.Rais yupo tayari kuhakikisha kwamba nguvu ya wananchi haipotei sasa tuonyeshe mfano kwa kuongeza kasi ya kujitegemea kwa kuweka miundombinu ya vyumba vya madarasa kwa watoto wa shule za msingi kuondoa msongamano darasani”, amesema Mbunge Mabula

Ndugu Aziza Isimbula, Katibu wa CCM Wilaya ya Ilemela amesisitiza kuhusu kuendeleza ushirikiano uliopo wa wananchi, ofisi ya mbunge na mkurugenzi  ili masuala ya maendeleo yazidi kuwa mepesi ambapo amewapongeza wananchi kwa kushiriki shughuli za maendeleo kwani wao  ni wadau wa kwanza wa miradi ya maendeleo,

Nae Mhandisi Modest Apolinary Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela amesema kuwa kupitia chanzo cha mapato ya ndani Manispaa ya Ilemela imetoa takriban kiasi cha Tsh. Milioni 72. 4 kwa ajili ya kukamilisha majengo mawili ya mama na mtoto katika zahanati za Ilemela na Nyakato ambazo zilikuwa zimekaa kwa muda mrefu bila kukamilika huku kiasi cha Tsh. Milioni 50 kimetolewa kwa ajili ya ujenzi wa jengo jipya la Wodi ya wazazi katika kituo cha Afya Buzuruga ambapo hadi sasa jengo lipo hatua ya boma.



Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.