• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

MADIWANI ILEMELA WAITAKA MWAUWASA KUTATUA KERO YA UKOSEFU WA MAJI

Posted on: August 12th, 2023

“Tunachotaka ni kuona wananchi wetu wanapata maji maana wasipopata maji uongozi wetu unakuwa hauna thamani yoyote tunawasaidiaje wananchi wetu?, Ilemela hakuna kijiji hoja ya msingi maji yawepo maeneo yote”


Ni Kauli iliyotolewa na Mhe. Hussein Magera Diwani wa Kata ya Ibungilo na Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma za Jamii akichangia hoja ya changamoto ya maji Wilayani Ilemela iliyoibuliwa kupitia maswali ya papo kwa hapo katika Baraza la Madiwani robo ya nne siku ya Tarehe 11 Agosti 2023.


Akichangia hoja hiyo Mhe Jonathan Mkumba diwani wa Kata ya Nyakato alisema kuwa mgao wa maji umegeuka kero zaidi hasa pale maji hayo yanapotoka usiku wa manane wakati watu wamelala na kuhoji maji yanapotoka usiku wa manane watachota saa ngapi?


Kwa upande wake Diwani kutoka Kata ya Buswelu Mhe Sarah Ng’hwani yeye alihoji juu ya ukosefu wa maji katika kata yake hali ya kuwa Wizara ilishatoa fedha kwa ajili ya utatuzi wa changamoto hiyo na kusisitiza kuwa anataka majibu sahihi ya kuwaeleza wananchi wake.


Katika Nyakati tofauti wakichangia hoja hiyo ya kero ya maji, Waheshimiwa Madiwani walisema kuwa MWAUWASA wamekuwa wakitoa ahadi ambazo hazitekelezeki hivyo kuwataka waje na majibu sahihi ya utatuzi wa kero hiyo ndani ya Wilaya ya Ilemela na kushauri iwapo MWAUWASA wameshindwa kutoa huduma hiyo ni vyema ikabinafsishwa ili wananchi waweze kutatuliwa kero hiyo.


“Ni wakati sasa wa MWAUWASA kuweka wazi tatizo ambalo linalopelekea changamoto hiyo ya maji kuwa kubwa Wilayani Ilemela na niwashauri mnapoongelea kuhusu uhaba wa maji ilemela muongelee kwa wilaya nzima na pia mje na majibu sahihi ili tatizo liweze kutatuliwa”amesema Mhe . Wilbard Kilenzi , diwani wa kata ya Ilemela.


Akijibu hoja hizo Mhandisi Stanley William, Meneja wa miundombinu MWAUWASA alifafanua juu ya kero hiyo ya maji na kukiri kuwa wamezidiwa kutokana na ongezeko la mahitaji ya maji katika jiji la mwanza kuwa kubwa ambapo mpaka sasa lita za ujazo milioni 160 zinahitajika kwa siku na uzalishaji wa sasa ni milioni 90 kwa siku


 “Upo upungufu wa maji kutokana na kuwa uzalishaji wa maji na mahitaji unatofautiana kwa kiasi kikubwa ndio maana tunategemea kukamilika kwa kituo cha Butimba kitakuja kupunguza adha ya maji kwani unataraji kuzalisha lita milioni 174, na ikiongezwa na kituo cha Kabangaja tatizo la maji litaisha kwani maji yatakuwa ya kutosha, tukiwa na maji ya kutosha wananchi wote watapata maji”, amesema Mhandisi Stanley


Kuhusu Kata ya Buswelu kukosa maji alifafanua kuwa hapo awali kulikuwa hakuna mabomba ya kutosha ya kuwafikia wananchi hivyo tenki la maji buswelu lilipokamilika  maji mengi yalikuwa hayana pa kwenda kufuatia hali hiyo, walitawanya maji kuwasaidia wananchi ambao walivuta mbali kuwasogezea laini karibu ili wapate presha ya kutosha pamoja na kuwafikia wananchi ambao hawakuweza kuvuta maji.


Mhandisi Stanley alihitimisha kwa kusema kuwa kuboreka kwa huduma ya maji Ilemela na Mwanza kwa ujumla ni baada ya kukamilika kwa mradi wa maji Butimba ifikapo oktoba 2023



Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.