• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

MADAWATI 710 YAKABIDHIWA KWA SHULE 33 ZA MSINGI ILEMELA

Posted on: October 3rd, 2022

Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, Mhe Hassan Masala amekabidhi jumla ya madawati 710 kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela ambayo yatatolewa kwa shule 33 za Msingi katika Manispaa hii ikiwa ni matokeo ya harambee iliyoratibiwa nae siku ya tarehe 31 Mei 2022.

Mhe, Masala akizungumza wakati wa zoezi hili amesema kuwa hii ni awamu ya pili ya utoaji wa madawati haya ambapo awamu ya kwanza yalikabidhiwa madawati 431 kwa shule 21 na awamu hii ya pili yamekabidhiwa  madawati 710 lengo kubwa ikiwa ni kupunguza changamoto za kujifunza na kujifunzia, kwa wanafunzi wa shule za msingi ilemela.


“Hatujisikii vizuri kama wazazi na viongozi tuliopewa dhamana ya kumsaidia Mhe Rais kuona watoto ya jamii ya watu tunayoiongoza wanakosa mazingira ya bora ya kupata  elimu na ndio maana tuliweka mkakati wa pamoja ambapo tuliwashirikisha wadau”, Mhe Masala amesema.


Aidha amesisitiza juu ya suala la ugawaji wa madawati haya kuzingatia usawa  na  kuwa isitokee upendeleo wa aina yoyote ile na madawati haya yatolewe kutokana na mahitaji ya maeneo husika kwa kuzingatia  shule zenye uhaba wa madawati.

Nae Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela Mhandisi Modest Apolinary mbali na kuwashukuru wadau mbalimbali waliochangia upatikanaji wa madawati haya,  amemshukuru Mkuu wa Wilaya kwa jitihada zake za kusaidia watoto wa Ilemela waweze kukaa na kupata maeneo ya kujifunzia huku akimuomba kuendelea kutumia wadau mbalimbali ikiwa ni pamoja  na kuendelea kuisimamia Wilaya ili kuweza kuileta maendeleo Wilaya ya Ilemela.


“Nikushukuru Mkuu wa Wilaya kwa jitihada hizi  zakusaidia watoto wa Ilemela waweze kukaa na kupata maeneo ya kujifunzia, pia  nikuombe uendelee kutumia wadau na kutusimamia ili tuweze kutekeleza wajibu wetu katika kuiletea maendeleo Wilaya yetu”, Mhandisi Modest amesema

Ndugu Yusuph Bujiku, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Ilemela, amepongeza jitihada hizi huku akiwataka wananchi kuwa mabalozi wazuri wa shughuli za serikali zinazofanyika, kwani haya yote yanayofanyika ni maono ya Mhe Rais yeye anatoa dira na anapotoa dira viongozi hutekeleza hivyo niwaombe wananchi tumpe ushirikiano kwa sababu kazi tunaziona na hivyo tuwe mabalozi wazuri wa kuwaeleza watu wengine kuwa serikali yetu inayo mambo inaendelea kufanya, amesisitiza


Akihitimisha zoezi hili la utoaji wa madawati Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilemela ametoa rai kwa watu wote kuhakikisha kuwa wanayatunza madawati hayo kwani ni lazima kuthamini na kutambua kuwa hizi ni fedha zilitolewa na wadau wa maendeleo. Huku akisisitiza suala la ushirikiano kwani haya yote yamewezekana kwa ajili ya ushirikiano uliopo chini ya kauli mbiu ya Ilemela isemayo, “Ilemela ni yetu Tushirikiane kuijenga”.





Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.