• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

MADAKTARI BINGWA WA DKT.SAMIA WAONGEZA UFANISI HUDUMA ZA AFYA

Posted on: June 21st, 2024

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela Bi.Ummy Wayayu  ametembelea kambi ya madaktari bingwa wa Dkt.Samia hospitali ya Wilaya ya Ilemela iliyopo mtaa wa Isanzu kata ya Sangabuye kuona namna huduma za kibingwa zinavyotolewa kwa ubora hali iliyopelekea ongezeko la wagonjwa wanaohitaji huduma za Afya na ushauri wa kitaalamu.

Akitoa taarifa ya zoezi linavyoendelea Mganga Mfawidhi wa hospitali ya Wilaya Ilemela Dr.Mateso Mayunga amesema huduma za kibingwa za magonjwa ya watoto, wanawake,upasuaji,magonjwa ya ndani na huduma za usingizi na ganzi salama zinaendelea kutolewa.

“ Mpaka sasa jumla ya wagonjwa 140 wameshahudumiwa ikiwa ni zaidi ya asilimia 100 ya wagonjwa wanaohudumiwa kwa siku katika hospitali yetu sambamba na makusanyo ya shilingi milioni 1.3 kwa siku nne za uwepo wa madaktari bingwa .”

Bi.Ummy amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuona umuhimu mkubwa wa wananchi wa kawaida kusogezewa huduma hizo za kibingwa.


Aidha madaktari hao wamewawezesha kwa vitendo madaktari wenyeji namna bora zaidi za kutoa huduma za afya kwa wananchi kwa kutumia vifaa bora na vya kisasa vilivyopo katika hospitali hiyo na kutoa maoni na mapendekezo ya aina ya vifaa na huduma za kuongezwa zaidi katika kuleta ufanisi ki utendaji.

“Tumefanikiwa kufanya oparesheni mbili kwa mafanikio makubwa,sisiti kusema kuwa hospitali hii inaweza kufanya makubwa zaidi ya haya kikubwa ni kubuni mbinu za namna ya kuwavutia wateja kwa kuboresha utoaji wa huduma zetu.” Dkt.Peter Kyamba bingwa wa upasuaji.

Nae Dkt.Irene Makundi bingwa wa magonjwa ya ndani amewataka wananchi kufika kwenye vituo vya kutolea huduma za afya kufuatilia kwa karibu afya zao kwani inaonyesha watu wengi ni wagonjwa na hawajijui.

“ Kwa siku hizi nne nimekuwepo hapa wagonjwa wengi wana shida ya presha,wanatembea na presha ipo juu sana wengine ipo chini na wanaendelea na shughuli zao hali ambayo ni hatari kiafya.”Dkt.Irene Makundi bingwa wa magonjwa ya ndani.

Madaktari hao wamepongeza mazingira ya usafi yaliyopo hospitalini hapo huku wakipongeza timu nzima ya watumishi kwa namna ambavyo wanafanya kazi kwa ushirikiano na kusisitiza uongozi wa Ilemela kuweka mazingira rafiki ya wananchi kufika kwa urahisi kupata kuhuduma za afya.

Mkurugenzi Ummy amepokea maoni na mapendekezo ya madaktari hao huku akiahidi kufanya maboresho ya miundo mbinu na huduma kwa wateja, kuongeza vifaa na dawa huku akithibitisha kuendelea kupokea fedha nyingi kutoka serikali kuu kwa ajili ya kuboresha huduma za afya ndani ya Manispaa yake.

Magdalena Shija ni mkazi wa mtaa wa Sangabuye,yeye ni mmoja wa wagonjwa waliopatiwa huduma ya afya na Dkt.Makundi anapongeza sana huduma nzuri aliyoipata na kuiomba serikali iendelee na utaratibu huo wa kusambaza madaktari maeneo ya nje ya miji kwani ni fursa kwa wananchi wa hali za chini kupata huduma.

Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.