• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

LISHE BORA KINGA YA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZA

Posted on: November 8th, 2023

Kuelekea maadhimisho ya wiki ya magonjwa yasiyoambukiza yanayoadhimishwa kila mwaka halmashauri ya manispaa ya Ilemela kupitia idara ya afya kitengo cha lishe imeanza  kutoa elimu ya lishe bora na namna ya kuepuka magonjwa hayo  kwa watumishi katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ilemela.


 Akizungumza wakati akifungua mafunzo hayo mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya hiyo ambaye pia ni katibu tawala wa Wilaya ya Ilemela Adv.Mariam Msengi amesema lishe ni moja kati ya vipaumbele muhimu katika serikali ya awamu ya sita kwa kutambua kuwa lishe bora ni chachu ya kuwa na wananchi waelewa na wenye manufaa makubwa kwa taifa lao.


“Tumeshuhudia mikataba mingi ya mambo ya lishe ikisainiwa katika ngazi za kitaifa ,hiyo yote inaonyesha kuwa Rais wetu anahitaji taifa lisonge mbele likiwa na wananchi wenye lishe bora sambamba na uwezo mkubwa wa kuchanganua mambo mbalimbali yenye tija.”


Akitoa elimu hiyo ya lishe bora Mratibu wa lishe wa Manispaa ya Ilemela Bi.Pili Khassim amesema kuwa magonjwa yasiyoambukiza yamekuwa mengi kwa sababu ya mitindo ya maisha tunayoishi na kuongeza kuwa ipo haja ya kubadili mitindo ya maisha yetu ya sasa ili kupambana na magonjwa yasiyoambukizwa kama vile magonjwa ya moyo na figo.


“Familia siku hizi zinaendeshwa na watoto badala ya wazazi /walezi kuziendesha.Watoto wakitaka chips,burger au pizza wanapewa wengine hata kila siku tunahisi tunaonyesha upendo kwa watoto bila kujua kuwa tunawapa lishe hatarishi kwa miili yao kutokana baadhi ya vyakula hivyo kuwa na mafuta mengi yasiyofaa.”


Bi. Pili amesisitiza watu kuzingatia lishe bora inayofaa kwa kula makundi matano ya vyakula ambayo ni vyakula vya nafaka,jamii ya kunde,mbogamboga,matunda,mafuta na sukari bila kusahau maji kwa kuzingatia mchanganyiko unaofaa.


Nae Afisa lishe wa Manispaa Bi.Joyce Albert ametoa elimu juu ya mitindo bora ya maisha kwa kuzingatia lishe bora yenye uwiano sahihi sambamba na kufanya mazoezi mepesi kama kutembea hali inayoweza kupunguza uwezekano wa kupata baadhi ya magonjwa kama kisukari,baadhi ya aina za saratani na shinikizo la damu.  


“Ili tupate kizazi bora ni lazima kuzingatia lishe bora hasa kwa watoto chini ya miaka miwili kwa kuzingatia ulaji unaofaa.” Amesema Bi.Joyce.


Neema Kipeja ni mmoja wa watumishi waliopata elimu hiyo ya lishe bora yeye anashukuru uongozi wa idara ya afya kwa kuona umuhimu wa kuanzia ndani katika kutoa mafunzo hayo.


" Somo la maandalizi ya chakula cha mtoto kwa kuchanganya nafaka chache au kutochanganya kabisa limekuwa zuri kwa kuzingatia kuwa wengine tuna watoto wadogo ambao bado hawajaweza kula wenyewe,kuzingatia usafi na ubora wa nafaka au vyakula kabla ya kuandaliwa ni muhimu kuepuka kula vyakula ambavyo vimeharibika.”


Sambamba na mafunzo hayo vipimo mbalimbali vya kiafya kama vile kupima uzito,urefu,hali ya lishe,kipimo cha presha na ushauri wa kiafya vilitolewa bure pamoja na zoezi la uchangiaji damu.


Maadhimisho hayo ya wiki ya magonjwa yasiyoambukiza kwa mwaka huu 2023 yamebebwa na kauli mbiu isemayo "usijisahau jali afya yako".



Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.