• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

LAAC yaridhishwa na utekelezaji na usimamiz wa miradi Ilemela

Posted on: March 24th, 2022

Kamati ya bunge ya kudumu ya hesabu za serikali za Mitaa (LAAC) ambayo imeongozwa na Makamu Mwenyekiti, Mhe Selemani Zedi (Mb), imeridhishwa na namna Manispaa ya Ilemela imekuwa ikisimamia na kutekeleza miradi mbalimbali ya Maendeleo ambapo wamekagua miradi miwili ambayo ni stendi mpya ya mabasi na maegesho ya malori pamoja na ujenzi wa Jengo la utawala.

Wakikagua mradi wa ujenzi wa jengo la utawala wamesema kuwa wamefarijika kukuta kuwa ujenzi huu umefikia asilimia 65, kwani mwaka 2019 walipokuja na kamati hii walikuta mradi umetelekezwa na mkandarasi (TBA) ambapo waliishauri Manispaa kuvunja mkataba na Halmashauri ikazingatia ushauri huu na sasa mradi upo hatua nzuri

“Niseme tu kwamba tofauti na kipindi kile tumekuja 2019 sasa hivi tunaona kwamba usimamizi wa shughuli za kimaendeleo, fedha za umma zinazoletwa kutekeleza miradi mbalimbali mkoani Mwanza umeboreka na kuimarika, hivyo kamati tumeridhishwa na maendeleo ya ujenzi huu ”, amesema Mhe. Selemani Zedi (Mb)

Waliongeza kusema kuwa wanayo imani kuwa kufikia mwezi wa sita jengo litakuwa limekamilika kwa asilimia 100 kama ambavyo taarifa imesomwa ili watumishi wapate sehemu nzuri ya kufanyia kazi na wananchi wapate huduma bora.

Kamati hiyo ilipata fursa ya kukagua stendi ya mabasi na maegesho ya malori iliyopo Nyamhongolo na kusema kuwa wameshuhudia ubora wa hali ya juu katika majengo yote waliyotembelea na kuwa wameridhishwa na namna Mkoa, Wilaya na Halmashauri inamsaidia Mhe Rais katika usimamizi na utekelezaji wa miradi.

“Huu mradi ni mkubwa sana na Shilingi Bilioni 26 ni fedha nyingi sana na mmezisimamia vizuri sana ni jambo la faraja kwamba thamani ya mradi mwanzoni ilikuwa ni shilingi Bilioni 28 lakini kwa usimamizi mzuri mmeweza kutekeleza mradi huu kwa shilingi bilioni 26 hivyo mmeokoa shilingi bilioni 2 kamati inawapongeza sana” Alisema Makamu Mhe Selemani Zedi(Mb)

Pamoja na kuipongeza Ilemela kwa utekelezaji mzuri wa miradi, wajumbe wa kamati hiyo ya Bunge walishauri kuwa itafutwe namna bora ya uendeshaji wa mradi wa stendi ya Mabasi na Maegesho ya malori kwa kuangalia wawekezaji wenye uwezo wa kuendesha biashara eneo hili, pamoja na hilo kuepusha kuwa na biashara ndani ya biashara na kuhakikisha kuwa stendi hii inaendeshwa  kidigitali ili mradi uwe endelevu na uweze kuleta tija kwani lengo kubwa la uanzishaji wa miradi hii ya kimkakati ni kuondoa utegemezi wa Halmashauri kwa serikali kuu.

Aidha zilitolewa pongezi kwa chuo kikuu cha Dar es Salam  kitivo cha uhandisi kwa kubuni mchoro wa jengo hili la stendi na maegesho pamoja na kusimamia hadi kukamilika, na kusema kuwa wanajivunia kwamba jengo hili limebuniwa na kusimamia na watanzania 

Nae Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi Robert Gabriel, aliishukuru kamati hiyo ya Bunge kwa kufika Mkoani Mwanza na kuahidi kupokea na kuyatekeleza maelekezo, maoni na ushauri wote utakaotolewa na kamati hii huku akisisitiza kuwa Mwanza haitakuwa sababu ya kukwamisha maelekezo ya serikali


“Mwanza haitakuwa sababu ya kukwamisha maelekezo ya serikali haitakuwa sababu ya kukwamisha ndoto na dira za mhe Rais, Mwanza haitakuwa kikwazo kutekeleza maelekezo na maagizo ya bunge la Jamhuri, Mwanza tumekubali kuleta mapinduzi na mageuzi kwa kutumia akili, utashi nguvu na maarifa hatutakubali Mwanza kuwa kichaka cha uharibifu, uovu na vurugu zaidi katika upande wa usimamizi wa miradi ya maendeleo”,Alisema Mhe Robert Gabriel






Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.