Wananchi mbalimbali waliofika katika stendi mpya ya mabasi ya Nyamhongolo wamepongeza jitihada za Serikali chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa hatua ya ukamilishaji wa stendi hii.
Katika nyakati tofauti wananchi waliofika katika stendi hii mpya kwa ajili ya kupata huduma ya usafiri wamepongeza kwa kusema kuwa ni stendi ya kisasa yenye mandhari nzuri ya kuvutia, eneo kubwa la kupumzikia wasafiri pamoja na kupaki magari tofauti na ilivyokuwa stand ya zamani ya mabasi ya Buzuruga, huku wakiiomba Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela kuzitatua changamoto ndogondogo ili kuweza kukidhi mahitaji ya wasafiri
Nao wafanyabiashara waliopo katika stendi ya Nyamhongolo wakiwemo wamepokea kwa furaha kuanza kutumika kwa stendi hii kwani kwao ni fursa kubwa kibiashara kwani kutawaongezea wateja huku wakishauri ikiwezekana iwe ni Stendi ya Mkoa ili kuwaongezea kipato chao huku wakihimiza ustaarabu katika matumizi ya stendi hii kudumishwa na kuahidi ushirikiano kwa Manispaa ya Ilemela.
Mhandisi Modest Apolinary, Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela amemshukuru Mhe. Rais Samia Suluhu kwa kutoa kipaumbele kwa Ilemela na kutoa fedha zilizofanikisha ukamilishaji wa stendi hii kubwa na ya kisasa huku akiwakaribisha wananchi kutumia fursa ya uwepo wa stendi hii kufanya biashara ili kuweza kuinua uchumi wa mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla
Stendi hii ambayo ilianza kujengwa mwaka 2019 na kukamilika mwezi wa nne mwaka 2022 imegharimu kiasi cha shilingi Bilioni 26. 6 za kitanzania fedha kutoka Serikali kuu ikiwa imegawanyika katika maeneo mbalimbali ikiwemo eneo la kuegesha malori takribani 80, eneo la stendi ya mabasi yenye uwezo wa kubeba mabasi 120, jengo la hoteli lenye vyumba 100, eneo la gereji, eneo la godown lenye uwezo wa kuchukua tani 5400, pamoja na maduka takriban 146.
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
Postal Address: 735 MWANZA
Telephone: + 255 736 200910
Mobile:
Email: md@ilemelamc.go.tz
Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.