• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

KLINIKI YA ARDHI KUPUNGUZA MALALAMIKO OFISI ZA WILAYA NA MIKOA

Posted on: September 13th, 2024

Zoezi la kusikiliza na kuzipatia ufumbuzi kero, malalamiko, changamoto na utoaji wa elimu juu masuala ya ardhi na ulipaji wa kodi zake maarufu kliniki za ardhi umesaidia kupunguza mlundikano wa wananchi katika ofisi za ardhi za wilaya ya Ilemela na mkoa wa Mwanza kwa ujumla


Hayo yamesemwa na kamishna wa ardhi msaidizi mkoa wa Mwanza Bi Happines Mtutwa wakati wa zoezi hilo katika ofisi za kata ya Pasiansi ambapo amefafanua kuwa zoezi la kliniki ya ardhi ni endelevu na limekuwa na manufaa makubwa siku hadi siku huku akiwataka wananchi kutoa ushirikiano


'.. Zoezi limeendelea kuwa la mafanikio makubwa sana, Hata ule mrundikano wa watu kwenye maofisi yetu umepungua sana, Zamani ilikuwa ukifika ofisini kwetu hata pale ofisi za ardhi manispaa ya Ilemela ilikuwa unakuta watu wengi sana kama  tupo kariakoo lakini siku hizi hauwezi kuliona hilo ..' Alisema


Aidha Bi Mtutwa ameongeza kuwa changamoto kubwa iliyosalia kwa sasa ni kero ya fidia ambayo nayo imeendelea kufanyiwa kazi na wakurugenzi wa halmashauri kwa kutenga fedha kwa awamu na kulipa wananchi waliotwaliwa maeneo yao na Serikali kwaajili ya shughuli mbalimbali za kijamii


Kwa upande wake afisa maendeleo ya ardhi manispaa ya Ilemela Bi Grace Isaac Masawe amesema kuwa wamesogeza huduma za ardhi karibu ya wananchi ili kuwarahisishia upatikanaji wa huduma kwa kuwa wapo wengine wagonjwa hawawezi kwenda maeneo ya mbali, wengine ni wazee na wengine ni masikini hawawezi kumudu gharama za kufata huduma ofisi za manispaa hivyo kufanikisha lengo la Serikali la kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na sahihi katika umbali mfupi na kwamba zaidi ya hati thelathini zimetolewa kwa wananchi wa kata ya Pasiansi sanjari na kuwaomba wananchi kujitokeza katika maeneo yao wanaposikia matangazo ya uwepo wa kliniki za ardhi


Mheshimiwa Rosemary Onesmo Mayunga ni diwani wa kata ya Pasiansi ambapo ameishukuru na kuipongeza Serikali kupitia wizara ya ardhi na wataalam wa ardhi manispaa ya Ilemela kwa kuweka utaratibu wa kufika katika maeneo ya wananchi na kutatua kero za wananchi kwani imeongeza imani ya wananchi kwa Serikali yao kwa kuwa wengi walikuwa wameshakata tamaaa baada ya kufuatilia huduma za ardhi kwa muda mrefu huku akiomba zoezi hilo kuwa endelevu


Nae mkazi wa Lumala Bi Eva Sylvester Agila amesema kuwa hatua ya ugawaji wa hati maeneo karibu na wananchi ni sahihi kwa wakati tulionao kwani hapo awali ilikuwa unafuatilia hati kwa muda mrefu na gharama kubwa za usafiri kufika ofisi za ardhi huku faida kubwa ya hati miliki ikiwa ni kuongeza thamani ya ardhi


Jumla ya hati thelathini zimekabidhiwa kwa wananchi wa kata ya Pasiansi na kamishina wa ardhi msaidizi mkoa wa Mwanza na kusikiliza kero na migogoro ya ardhi kwa wananchi sambamba na kutoa elimu ya masuala ya ardhi

Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.