• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

KAYA 200 ZAFUZU MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASIKINI (TASAF) ILEMELA

Posted on: July 4th, 2024

Jumla ya kaya elfu mbili kati ya kaya elfu tano mia tatu arobaini na tisa zimefuzu na kuondolewa katika mpango wa kunusuru kaya masikini kwa wilaya ya Ilemela


Hayo yamebainishwa na mratibu wa mpango wa kunusuru kaya masikini TASAF Ndugu Leonard Robert ambapo amesema kuwa mwaka 2023 mfuko wa maendeleo ya jamii TASAF ulitoa taarifa na kufanya zoezi la tathimini kwa walengwa ili kubaini kaya zilizoimarika kiuchumi na kukidhi vigezo vya kuondolewa kwenye mpango ambapo kwa wilaya ya Ilemela jumla ya kaya 3,349 zitaendelea kupokea malipo kutoka kwenye mpango huku akizitaka kaya imarika kuendelea kukutana katika vikundi na kupanga mipango na mikakati ya kujiendeleza kiuchumi


‘.. Kuondolewa katika mpango haimaanishi kwamba vile vikundi vyetu vya TASAF vimekufa, kaya zilizoimarika zinaweza kuendelea kukutana na zikatumia vikundi hivyo kupanga mipango ya kujiendeleza kiuchumi hata kunufaika na mikopo ya halmashauri kupitia mapato yake ya ndani ..’ Alisema


Aidha Ndugu Leonard akaongeza kuwa zoezi la kubaini kaya zilizoimarika kiuchumi ni endelevu na kaya zitakuwa zikiondolewa kwa kadri ya zinavyofuzu katika mpango


Mkama Costantine Sururu ni mwezeshaji wa TASAF manispaa ya Ilemela katika kata ya Buzuruga ameshauri kaya zilizobaki na kuendelea na kunufaika na mpango kutumia fedha wanazopewa kwaajili ya shughuli za kiuchumi kwaajili ya kujiongezea kipato kwa kuwa ipo siku nao watatoka katika mpango sanjari na wale waliotoka kutumia fursa ya vikundi kukopa katika taasisi za fedha na halmashauri kama njia ya kujiimarisha kiuchumi


Nae mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa ustawi kata ya Buzuruga Ndugu Bahati Richard Kabadi mbali na kumshukuru Rais Mhe Dkt Samia Suluhu Hasan kwa mpango huo wa kupunguza umasikini, akazipongeza kaya zilizotoka katika mpango wa kunusuru kaya masikini kwani walitumia vizuri fedha walizopata kwaajili ya shughuli za uzalishaji mali na kujiimarisha kiuchumi huku akisisitiza kaya zilizosalia kuiga mfano huo


Kwa upande wake Bi Pili Mtatiro Masigiti ambae ni miongoni mwa wana kaya zilizofuzu mpango kutoka mtaa wa Nyambiti ametaja faida alizozipata kutokana na TASAF ikiwemo kusomesha watoto na wajukuu zake, kukarabati nyumba yake, kuwa na uhakika wa chakula cha kila siku na kupata mtaji wa biashara tofauti na hali ya kiuchumi aliyokuwa nayo kabla ya kuwepo katika mpango


Manispaa ya Ilemela katika malipo ya dirisha la mwezi machi-aprili inatarajia kufanya  malipo ya jumla ya kiasi cha Tshs  235,176,000 (Shilingi Milioni 235.17) kwa njia ya fedha taslimu, njia ya mtandao wa simu na benki kwa kaya 5349 zinazonufaika na mpango wa kunusuru kaya masikini ikiwa ni pamoja na kaya zilizofuzu mpango ambapo haya yatakuwa malipo yao ya mwisho kabla ya kuondolewa


Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.