• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Kamati za Ujenzi zaaswa kuacha malumbano ukamilishaji wa madarasa

Posted on: November 18th, 2021

Na Yusuph Ludimo, Ilemela

Kamati za ujenzi wa madarasa yanayotokana na fedha za mpango wa maendeleo dhidi ya UVIKO-19 zilizotolewa hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hasan zimetakiwa kuacha malumbano na vikwazo visivyo vya lazima ili kukamilisha kwa wakati ujenzi wa miundombinu hiyo ndani ya muda uliopangwa


Rai hiyo imetolewa na Mbunge wa Jimbo la Ilemela Mhe Dkt Angeline Mabula wakati wa ziara yake ya kukagua hatua za ujenzi katika shule mbalimbali zilizopo ndani ya manispaa ya Ilemela ikiwemo Kilimani sekondari, Kisundi sekondari, Bugogwa sekondari, Lumala sekondari, Shibula sekondari, Lukobe sekondari, Kabuhoro sekondari na Mwinuko sekondari  ambapo akawataka wajumbe wa kamati hizo kuwa wazalendo kwa kuweka maslahi ya taifa mbele badala ya matamanio binafsi ili kukamilisha ujenzi huo ndani ya muda uliopangwa kwa kuzingatia ubora na ufanisi unatakiwa

‘.. Tumepita baadhi ya shule unakuta wajumbe wa kamati za ujenzi wanadai posho, kwengine hakuna ushirikiano kila mmoja ana lake, Sasa hatuwezi kufika kwa namna hii, lazima tuwe wamoja tuache malumbano ..’ Alisema


Aidha Mhe Dkt Mabula mbali na kumshukuru Rais Mhe Samia Suluhu Hasan kwa kutoa fedha hizo zitakazo saidia kupunguza changamoto ya upungufu wa madarasa na ile ya watoto kufata elimu katika umbali mrefu amewapongeza baadhi ya wakuu wa shule na kamati zao kwa ubunifu  na matumizi sahihi ya fedha hizo kwa kujibana na kuongeza miundombinu ambayo haikuwepo katika maelekezo ya matumizi ya fedha  hizo ikiwemo uongezaji wa madarasa na ofisi huku nyengine zikiwa katika hatua nzuri katika ukamilishaji wake


Kwa upande wake meya wa manispaa ya ilemela Mhe Renatus Mulunga amefafanua kuwa manispaa yake imetengewa kiasi cha shilingi bilioni moja na milioni mia tisa na arobaini na mpaka sasa wameshapokea bilioni moja na milioni mia nane na arobaini kwaajili ya ujenzi wa madarasa huku akiahidi kusimamia matumizi ya fedha hizo na uzingatia wa ubora wa kazi itakayofanyika


Majaliwa Gerana ni Mwalimu Mkuu wa shule ya sekondari Kilimani iliyopo kata ya Kawekamo ambae amefananua kuwa mbali na kukamilisha hatua ya upauaji wa madarasa mawili yaliyokuwa yamepangwa kujengwa katika shule yake amekumbana na changamoto mbalimbali katika ujenzi huo ikiwemo upandaji wa bei za vifaa vya ujenzi na upatikanaji wa shida wa baadhi ya vifaa ikiwemo saruji kutokana na kuhitajika na watu wengi

Manispaa ya Ilemela inatarajia kufika tamati ya ujenzi wa madarasa ifikapo Desemba 15, 2021 ambapo kila shule itatakiwa kuwa imekamilisha ujenzi huo kwaajili ya kupokea watoto wa kidato cha kwanza kwa mwaka mpya wa masomo.

Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.