• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Kamati za kudumu za Halmashauri zahitimisha ziara robo ya pili 2020/2021

Posted on: February 16th, 2021

Ikiwa ni robo ya pili kwa mwaka wa fedha wa 2020/2021 waheshimiwa madiwani wakiwa katika kamati wanazohudumu wameweza kutembelea na kukagua miradi inayoendelea kutekelezwa katika Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

Kwa upande wa kamati ya Huduma ambayo walitembelea miradi ya ujenzi wa madarasa lengo haswa ikiwa ni kufuatilia ukamilishaji wa miundombinu mbalimbali ambayo inahusika na utoaji wa huduma za kijamii.Katika ziara ya robo ya pili wajumbe wa kamati hii waliweza kukagua ukamilishaji wa ujenzi wa miundombinu ya  madarasa katika shule za sekondari ikiwa ni pamoja na kukagua maendeleo ya ujenzi wa shule mpya. Walipata pia fursa ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la wakinamama kwa ajili ya kujifungulia lililopo zahanati ya nyakato.Pia waliweza kukagua soko lililopo nyasaka kwa ajili ya kuangalia namna ambayo wataweza kuboresha miundominu ya soko hili ili liweze kuboreshewa miundombinu kwa ajili ya kutumika na wafanyabiashara. Pamoja na kufanya ukaguzi huo walisisitiza suala la ukamilishaji wa miundombinu ya madarasa ili kuweza kuendana na agizo la Waziri Mkuu huku wakisisitiza ukamilishaji wa miradi mbalimbali ili kuweza kuboresha utoaji huduma kwa wananchi.

Kamati ya Mipangomiji nayo ilipata fursa ya kukagua miradi ambayo inasimamiwa na kamati hiyo ikihusiana na suala la zima la ujenzi, ardhi na mipangomiji. Wakiwa katika ziara hiyo waliweza kutembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa Stendi ya mabasi na uegesheji wa malori Nyamhongolo ambapo walipongeza na kushauri kuwa ufuatiliaji ufanyike ili pesa iletwe kwa wakati kwa ajili ya kuweza kukamilisha ujenzi huo kwa wakati. Aidha waliweza kufuatilia masuala ya migogoro ya ardhi katika manispaa na kuwataka wataalamu wa Idara ya Mipangomiji wanatatua migogoro hiyo ili kuondoa kero kwa wananchi

Ziara za robo ya pili kwa mwaka wa fedha 2020/2021 zilihitimishwa na Kamati ya Fedha ambapo wajumbe wa kamati hiyo waliweza kukagua mialo katika Manispaa ya Ilemela kwa ajili ya kusikiliza changamoto za wavuvi ikiwa uvuvi ni chanzo kikuu cha mapato cha Ilemela, aidha waliweza kukagua maendeleo ya ukarabati wa mzani wa kupimia magari yanayopitisha mazao ya uvuvi uliopo mwaloni kirumba.Kamati hiyo pia iliika kukagua maendeleo ya ujenzi ya mabweni mawili ya wasichana katika shule za sekondari Bwiru wasichana na Buswelu huku wakiagiza kuhakikisha kuwa mabweni yanakamilika ili kuweza kuanza kutumika.

Ziara hizi za kamati za kudumu hufanyika katika kila robo na lengo kuu ni kufuatilia utekelezaji wa shughuli za maendeleo za Halmashauri kwani kamati hizi za kudumu zinao wajibu wa kuishauri halmashauri kutengeneza malengo yanayozingatia matakwa ya Miji na kuchukua, hatua ambazo zitaonekana zinafaa ili kufikia malengo yaliyokusudiwa. Aidaha kamati hizi hushauri Halmashauri kufanya maamuzi juu ya Sera muhimu pamoja na kuishauri Halmashauri kufanya maamuzi juu ya utoaji wa huduma kulingana na rasilimali zilizopo.

Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.