• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

KAMATI ZA HUDUMA ZA MIKOPO NGAZI YA KATA ZIMETAKIWA KUSIMAMIA UTOAJI WA MIKOPO

Posted on: October 22nd, 2024

Kamati za huduma za mikopo ngazi ya kata zimetakiwa kusimamia suala zima la utoaji wa mikopo kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kuanzia hatua ya uundaji wa vikundi sambamba na uibuaji wa miradi pamoja na kufuatilia miradi inayoenda kutekelezwa ili iweze kuleta tija katika kufanikisha dhana inayotarajiwa ya kuwainua kiuchumi.


Rai hiyo imetolewa na Bi Ummy Wayayu ambae ni mkurugenzi wa manispaa ya Ilemela alipokuwa akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo wajumbe wa kamati hizo.


“Utoaji wa mikopo hii ni utekelezaji wa sera, mikakati na mipango ya taifa katika kupunguza umaskini, kwahiyo tunapoenda kutoa mikopo hii tukalenge katika kupunguza umaskini na si vinginevyo”, amesema Bi Ummy


Kupitia mafunzo haya wajumbe wa kamati hizo wamepitishwa katika muongozo na kanuni za utengaji, utoaji na usimamizi wa mikopo ya vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu katika mamlaka za serikali za mitaa ya mwaka 2024.


Akifafanua juu ya muongozo na kanuni hizo, Bi Amina Bululu ambae ni mratibu wa mikopo kwa vikundi manispaa ya Ilemela amesema kuwa, zoezi la utoaji wa mikopo kwa vikundi litafanyika kielektroniki kupitia mfumo wa maombi ya mikopo na kwamba kikundi hakitaruhusiwa kuomba mkopo mpya kama kina deni la zamani.


Aidha Bi Amina amefafanua zaidi kwa kusema kuwa kutakuwa na kamati za utoaji wa mikopo kwa ngazi za mkoa, wilaya na kata na kwamba utengaji, utoaji na urejeshaji wa mikopo utafanyika kwa utaratibu wa 4;4;2 kwa maana ya kuwa asilimia nne kwa wanawake, asilimia nne kwa vijana na asilimia mbili kwa watu wenye ulemavu


Bi Imelda Chundu ni mtendaji wa kata ya Mecco mbali na kushukuru kwa mafunzo hayo ameomba kupatiwa nyaraka zitakazomsaidia katika utekelezaji wa shughuli za kila siku za mikopo kama hadidu rejea huku Bwana Mponeja Katemi ambae ni mtendaji wa kata ya Kayenze akitaka kutengwa kwa bajeti ya uendeshaji wa shughuli za mikopo kwa ngazi ya kata


Akifunga mafunzo hayo kaimu mkuu wa idara ya maendeleo ya jamii manipsaa ya Ilemela Bi Florence Vedasto amewataka watumishi wa umma kutojihusisha na mikopo hiyo na kwamba kufanya ubadhirifu wowote ni kosa kisheria hivyo hatua kali zitachukuliwa kwa yeyote atakaebainika kuhujumu juhudi hizo za serikali katika kuwaondolea wananchi wake umasikini


Kamati ya huduma za mikopo ngazi ya kata inaundwa na mtendaji wa kata, afisa maendeleo ya jamii wa kata, afisa ustawi wa jamii, afisa elimu kata, maafisa ugani wa kata, watendaji wa mitaa ya kata husika pamoja na polisi kata.

Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.