• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

KAMATI YA SIASA WILAYA YA ILEMELA YARIDHIISHWA NA UTEKELEZAJI MZURI WA MIRADI

Posted on: February 20th, 2020

Kamati ya siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Ilemela ikiongozwa na Mwenyekiti Ndugu Nelson Mesha, imeipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela kwa utekelezaji mzuri wa miradi ya Maendeleo.

Pongezi hizo wamezitoa walipofanya ziara kwa ajili ya kutembelea, kukagua na kufuatilia utekelezaji wa miradi ya maendeleo.


Ndugu Nelson Mesha ambae ni Mwenyekiti wa kamati hiyo alielekeza pongezi zake kwa Mkurugenzi na uongozi wa Manispaa ya Ilemela kwa utekelezaji mzuri wa miradi yenye viwango na kusema kuwa Ilemela imekuwa ikisimamia na kutekeleza vizuri Ilani ya Chama cha Mapinduzi tangu mwaka 2015 kwani changamoto zilizokuwepo hapo awali ni tofauti na zilizopo sasa mambo mengi yameboreshwa ikiwemo utatuzi wa changamoto za migogoro ya ardhi.


Aidha akiwa katika ukaguzi wa mradi wa maji katika Tanki la maji Iramba lililopo Kata ya Nyamhongolo alisema kuwa, amesikitishwa kwa kutokukamilika kwa mradi huo na hivyo kutoa rai kwa MWAUWASA kuhakikisha kuwa mradi huo na mingine inakamilika ili uweze kuondoa changamoto ya upatikanaji wa maji kwa wananchi wa eneo hilo la Nyamhongolo na maeneo ya jirani.


   “Nitoe rai kwa MWAUWASA kuhakikisha wanakamilisha mradi huu wa maji na miradi mingine ili wananchi waondokane na adha ya upatikanaji wa maji safi na salama”, alisisitiza


Nae Mbunge wa Ilemela Dkt.Angeline Mabula alisisitiza kuhusu suala la maji kwa kuwataka MWAUWASA kuongeza kasi ya usimamizi wa miradi inayoendelea ili kuondoa adha ya maji kwa wananchi kwani hitaji la maji kwa wananchi wa Manispaa ya Ilemela ni Kubwa.


Nae Katibu wa kamati hiyo ya Siasa ya Wilaya, Aziza Isimbula aliipongeza Ilemela kwa kusema kuwa huwezi kuwa na miradi mizuri yenye tija kama hakuna usimamizi mzuri unaozingatia thamani ya fedha. Aliongeza kusema kuwa miradi hii waliyotembelea itakapokamilika italeta taswira nzuri kwa Manispaa ya Ilemela.


Pamoja na pongezi hizo wajumbe wa kamati hiyo walitoa maoni mbalimbali kuhusiana na miradi hiyo waliyotembelea pamoja na kutoa ushauri kwa ajili ya kuboresha hatua mbalimbali za miradi ilipofikia ili iweze kuleta tija kwa wananchi wa Ilemela.


Kamati ikiendelea na  ziara hiyo ilitembelea mradi wa kimkakati wa stendi ya mabasi na eneo la maegesho ya malori eneo lililopo katika kata ya Nyamhongolo ambapo walipongeza jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt John Pombe Magufuli kwa kutoa fedha kuweza kutekeleza mradi mkubwa kama huo ambapo ukikamilika utaleta taswira nzuri kwa Manispaa ya Ilemela pamoja na kuongeza mapato ya Halmashauri.

Pamoja na hayo Mhe.Angeline Mabula ambae pia ni mbunge wa Jimbo la Ilemela alisema kuwa ana imani mradi huu utakapokamilika uchumi wa Ilemela utaenda kuimarika. Aidha alitoa ushauri kwa mkandarasi wa mradi huo STECOL Corporation Ltd kuwa kazi katika mradi huo zifanyike kwa awamu yaani mchana na usiku ili kuweza kukamilisha mapema kwani lengo ni kuona mradi unaanza kufanya kazi ili kuharakisha maendeleo kwa wananchi wa Ilemela.

Aidha Ndugu Mesha amemtaka mkandarasi wa mradi kuhakikisha kuwa wanaboresha malipo ya vibarua wanaofanya katika mradi huo kwani kazi inayofanyika hapo ni kubwa ukilinganisha na malipo hayo ambayo hayaendani na kiwango cha malipo ya serikali kwa vibarua.

Nae Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilemela, Mhe Renatus Mulunga alitoa pongezi zake kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano, Mbunge wa Ilemela na timu ya wataalam wa Manispaa ya Ilemela na wananchi kwa jitihada zao walizowekeza katika kuhakikisha kuwa miradi inakamilika kwa viwango vya juu.


Kamati ya siasa ya CCM wilaya ya Ilemela imekagua miradi 10 inayotekelezwa na Manispaa ya Ilemela ikiwa ni utaratibu waliojiwekewa kwamba kila baada ya miezi 6 hufanya ukaguzi huo kuangalia utekelezaji wa Ilani ya Chama cha Mapinduzi.


Miradi waliyotembelea na kukagua ni; mradi wa mzani wa mazao ya samaki, Barabara za Mwaloni, mjimwema –Bigbite, Sabasaba-kiseke-buswelu, Mradi wa bwalo la chakula katika shule ya sekondari Buswelu, mradi wa kimkakati wa stendi ya mabasi Nyamhongolo, Kituo cha polisi Nyamhongolo, tanki la maji Iramba na mradi wa ujenzi wa nyumba ya mwalimu shule ya msingi Nyamadoke.



Nyumba ya mwalimu shule ya msingi Nyamadoke


Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.