• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Kamati ya fedha Ilemela yakagua miradi kujiridhisha na matumizi bora ya fedha

Posted on: October 22nd, 2021

Kamati ya fedha na mipango ya Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela imefanya ziara ya kutembelea na kukagua miradi mbalimbali ndani ya manispaa hiyo lengo likiwa ni kujiridhisha na matumizi ya  fedha  zinazotolewa na kuelekezwa kwenye miradi ya wananchi wa Ilemela.

Akizungumza wakati wakikagua mradi wa ukarabati wa ofisi na vyoo vya mwalo wa Kayenze Mwenyekiti wa kamati hiyo ambaye pia ni Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilemela Mhe.Renatus Mulunga amesema ni wajibu wa kamati hiyo kufanya ufatiliaji wa mara kwa mara punde fedha zinapotoka kwa ajili ya kukagua thamani ya fedha inayotumika katika miradi mbalimbali ya maendeleo ili iweze kuleta tija kwa wananchi.

Aidha kamati imetembelea mradi wa ofisi ya serikali ya mtaa Kayenze ambayo imekaribia kukamilika ambapo ujenzi wake umegharimu kiasi cha shilingi milioni 8 ikiwa ni fedha kutoka chanzo cha mapato ya ndani.

Wakiwa katika eneo la ujenzi wa kituo cha afya Kayenze, Mhe.Mulunga amesema “Tumepokea milioni 250 kutoka serikali kuu za hatua ya awali kuanzisha ujenzi huu,hakika tunaishukuru serikali ya awamu ya sita kwa kuonyesha nia ya moja kwa moja kuanzisha na kumaliza miradi ya afya kama hii kwa manufaa ya wananchi wake,kikubwa tunataka fedha hii itumike kwa uangalifu kwa malengo yaliyokusudiwa.”

Miradi mingine iliyotembelewa ni pamoja na ujenzi wa bweni shule ya sekondari Sangabuye ambapo kazi inaendelea vizuri ,soko la Kiloleli,Nyasaka na Kabwaro sambamba na ujenzi wa ofisi ya serikali ya mtaa Nyambiti.

Aidha, kamati hiyo ilitoa pongezi kwa timu ya masoko ya manispaa kwa kazi kubwa wanayoendelea nayo ya kuwapanga na kuwahamishia wafanyabiashara katika  maeneo rasmi ya masoko na pongezi hizo wamezitoa walipotembelea masoko yaliyoainishwa kwa ajili ya kuwapanga wafanyabiashara hao

Mstahiki meya alionyesha msisitizo kuhusu suala la kuwapanga wafanyabiashara  kwa  kuwahimiza waheshimiwa  kuungana ili kuweza kufanikisha kwani kwa sasa suala hili ni kipaumbele kwa sasa kufuatia agizo la mMhe. Rais.

Manispaa ya Ilemela inaendelea na maboresho ya miundo mbinu ndani ya masoko yake yote kwa kasi sambamba na uwekaji wa taa ili kuweza kuruhusu biashara kufanyika hadi nyakati za usiku lakini pia ikiwa ni moja ya njia ya kuimarisha ulinzi wa mali za wafanyabiashara wake, utengenezaji wa vyoo,umwagaji wa molamu maeneo korofi na kuendelea na masuala ya ufatiliaji wa ruti za magari ya abiria kufika hadi jirani au ndani ya maeneo ya masoko yote rasmi.




Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.