• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

Jamii yatakiwa kuunga mkono shughuli za maendeleo

Posted on: April 21st, 2022

Jamii imetakiwa kushiriki na kuunga mkono utekelezaji wa shughuli mbalimbali za kimaendeleo zinazoendelea katika maeneo yao.


Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa wilaya ya Ilemela Mhe Hasan Elias Masala wakati wa uzinduzi wa ujenzi wa bweni la wanafunzi  wenye ulemavu na mahitaji maalum iliyofanyika katika viwanja vya shule ya msingi Buswelu wilayani humo litakalo gharimu kiasi cha shilingi Milioni mia moja na hamsini kwa ajili ya kuhudumia wanafunzi arobaini ambapo ameiasa jamii kuunga mkono jitihada za Serikali kwa kushiriki ujenzi wa miradi mbalimbali ya kimaendeleo inayotekelezwa katika maeneo yao kwa kuilinda, kuchangia nguvu na mali ili iweze kukamilika kwa wakati‘.. Natoa pongezi kwa wote walioibua wazo hili na wadau waliotoa michango yao ili kuwezesha kuanza kwa ujenzi, Niwaombe tusimamie vizuri michango yote inayotolewa ili tuweze kukamilisha mradi huu kwa wakati ..’ Alisema


Aidha Mhe Masala mbali na kumshukuru Rais wa Jamahuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hasan kwa jitihada zake katika kuboresha sekta ya elimu amewapongeza Mbunge wa Jimbo la Ilemela Mhe Dkt Angeline Mabula kwa kuunga mkono jitihada hizo ambapo ametoa jumla ya tofali elfu tano na mkurugenzi wa manispaa hiyo aliyetoa tofali elfu tano mia tisa na ishirini kwaajili ya ujenzi huo huku akiwataka wadau walioahidi kuchangia gharama za ujenzi wa bweni hilo kuhakikisha wanakamilisha ahadi zao ndani ya siku saba ili kuharakisha ujenzi wa mradi huo.



Kwa upande Mkurugenzi wa manispaa ya Ilemela Mhandisi Modest Joseph Apolinary amewataka wazazi kuhakikisha wanawafichua watoto wenye ulemavu na kuwapeleka shuleni ili waweze kupata elimu itakayosaidia kuboresha maisha yao na nchi kwa ujumla huku akiahidi ushirikiano katika kuhakikisha mradi huo unakamilika kwa wakati na kupunguza kero ya muda mrefu ya ukosefu wa mabweni kwa shule zenye wanafunzi wenye mahitaji maalum .

Sara Ng’wani ni diwani wa kata ya Buswelu amemshukuru mkuu huyo wa wilaya kwa jitihada zake katika kusimamia utekelezaji wa shughuli za maendeleo huku akiahidi kuchangia kiasi cha shilingi laki mbili kama ishara ya kuunga mkono juhudi hizo.



Akihitimisha mkuu wa shule ya Buswelu Mwalimu James Wanchala amesema kuwa wadau mbalimbali wamechangia ujenzi wa bweni hilo wakiwemo chama cha walimu wilaya ya Ilemela, maafisa elimu kata, watumishi wa idara ya elimu kutoka makao makuu, walimu wakuu wa shule binafsi na zile zenye vitengo ambapo jumla ya shilingi milioni kumi na moja na laki tatu na elfu tisini na tano zimeshakusanywa kwaajili ya ujenzi wa bweni hilo.

Announcements

  • TANGAZO LA KAZI NAFASI YA UDEREVA DARAJA LA II June 04, 2025
  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • KAMPENI YA KITAIFA YA UTOAJI WA MATONE YA VITAMI A YAFIKIA ASILIMIA 98.7

    June 26, 2025
  • WENZA WA VIONGOZI WATEMBELEA SEKONDARI YA IGOGWE WAPONGEZA JUHUDI ZA SERIKALI

    June 26, 2025
  • DAWATI LA HUDUMA ZA USTAWI WA JAMII KUENDELEA KUIMARISHA UTOAJI WA HUDUMA STENDI YA MABASI NYAMHONGOLO

    June 26, 2025
  • ILEMELA YAPONGEZWA KUPATA HATI SAFI, WITO WATOLEWA KUTOZALISHA HOJA MPYA ZA UKAGUZI

    June 17, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.