• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

JAMII YATAKIWA KUTUNZA NA KULINDA ZIWA VIKTORIA

Posted on: March 29th, 2023

Jamii imetakiwa kutunza na kulinda Ziwa Viktoria na mazingira yake ili liweze kuwa na manufaa kwa kizazi cha sasa na cha baadae


Rai hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Jumuiya ya halmashauri zinazozunguka Ziwa Viktoria LAVRAC ambae pia ni Mstahiki meya wa manispaa ya Musoma Mhe William Gumbo ambapo ameupongeza uongozi wa ushirika wa wavuvi maarufu BMU wa kata ya Bugogwa unaosimamia mwalo wa Igombe kwa juhudi zao katika kuhakikisha mwalo huo unakuwa safi pamoja na kusisitiza kuwa ziara iliyofanywa na ushirika huo wa mamlaka za Serikali za mitaa ni sehemu ya uhamasishaji juu ya umuhimu wa kutunza Ziwa hilo na kulilinda

“Niwapongeze kwa utunzaji wa mazingira kiukweli mwalo ni msafi sana, Lakini hili lisiishie leo tuendelee kutunza Ziwa na mazalia yake”,  amesema


Aidha Mhe Gumbo ameishukuru benki ya NMB kwa ufadhili wa tukio hilo sanjari na kuomba wadau wengine kuendelea kuunga mkono Serikali katika kulinda na kutunza mazingira


Kwa upande wake mwakilishi wa Mstahiki meya wa manispaa ya Ilemela ambae pia ni diwani wa kata ya Mecco Mhe Godlisten Kisanga mbali na kuwapongeza wananchi kwa ushirikiano wao katika zoezi la usafi amewaalika viongozi na wanachama wa jumuiya ya LVRAC kuwekeza wilaya ya Ilemela kwani wilaya hiyo ina maeneo mengi na fursa lukuki za kiuchumi


Nae meneja mwandamizi mahusiano na biashara za Serikali kutoka benki ya NMB Bwana Adelard Mang'ombe amesema kuwa benki yake mbali na utaratibu wa kawaida wa kurudisha sehemu ya faida wanayoipata kwenda kwa wananchi maarufu CSR, Benki yake imeongeza bilioni 2 katika bajeti yake kwaajili ya usafi na mazingira hivyo tukio lililofanyika leo ni sehemu ya kampeni wanazoziunga mkono juu mazingira



Nyabugumba Jonathan ni afisa mazingira wa manispaa ya Ilemela, Yeye amewasisitiza wananchi waliojitokeza katika tukio hilo kulifanya zoezi la usafi kama sehemu ya utamaduni wao na sio kusubiria kuhimizwa

Manispaa ya Ilemela imekuwa mwenyeji wa mkutano mkuu wa jumuiya ya halmashauri zinazozunguka Ziwa Viktoria kwa mwaka wa 2023 ambapo shughuli za kufanya usafi katika mwalo wa Igombe na upandaji miti katika kituo cha afya Karume zimefanyika ikiwa ni sehemu ya shughuli zilizopangwa kufanyika na jumuiya hiyo kabla ya mkutano wake mkuu wa mwaka utakaofanyika kesho katika ukumbi wa Rock City Mall Ilemela jijini Mwanza na kuhudhuriwa na halmashauri zote wanachama  wa nchi za Kenya, Uganda na Tanzania mwenyeji





Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.