• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

JAMII YAASWA KUPINGA UKATILI WA AINA ZOTE

Posted on: December 2nd, 2022

Jamii ya Ilemela imeaswa kuendelea kupinga ukatili wa aina zote unaotokea katika familia kwa kuzingatia kuwa asilimia kubwa nguzo ya familia ambayo ni mwanamke huwa ni muathirika namba moja sambamba na watoto.Jamii inatakiwa kumlinda na kumjali mwanamke kwa ustawi wa familia nzima.


Hayo yamesemwa na mgeni rasmi ndugu Isack Ngasa afisa maendeleo ya jamii Mkoa wa Mwanza katika kongamano la wanawake wa Ilemela kuelekea maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili duniani yanayoadhimishwa kuanzia Novemba 25,2022 hadi Disemba 10,2022 lililoandaliwa na shirika lisilo la kiserikali linalojihusisha na masuala ya kupinga ukatili kwa wanawake na watoto KIVULINI-Mwanza



Akizungumza wakati wa kongamano hilo ndugu Isack amesema serikali ya Tanzania inayoongozwa na Mhe.Dkt Samia Suluhu Hassan inatambua umuhimu wa mwanamke katika jamii ndio maana zipo jitihada za kumwezesha na kumuinua mwanamke kiuchumi ili kusimama vema kwa nafasi yake.


“Mwanamke ndie mwenye nafasi ya kuokoa taifa kwa kuzingatia kuwa ndiye anayejihusisha moja kwa moja na malezi na makuzi ya watoto,serikali imeanzisha jitihada za makusudi za kumuinua mwanamke kiuchumi kwa kutoa mikopo na kuboresha na kuanzisha shule maalum kwa ajili ya watoto wa kike lengo likiwa kumuongezea nguvu na uwezo  vyenye kuleta matokeo chanya kwa kuzalisha familia bora.”Amesema Isack



Nae Mkurugenzi wa shirika la KIVULINI ndugu Yassin Ally amesema wazazi na walezi wanapaswa kuwa makini na namna watoto wanavyojihusisha na mambo mbalimbali ya mitandao ya kijamii kwani wengi hupenda kuiga vitu bila kufikiria madhara yake baadae.


“Masuala ya mitandao ya kijamii yanaendelea kuingiza tamaduni za mataifa mengine ambazo watoto wanaiga kwa kutenda na madhara yake tunaanza kuyaona,mambo ya kulawiti,ushoga ni baadhi ya mambo watoto wetu wanaiga huko.Wazazi tuwasaidie watoto wetu kuiga mambo yenye manufaa kwao na si kila kitu .”Amesema Yassin



Aidha mwakilishi wa umoja wa wanawake wa CCM (UWT) Ilemela Bi.Herith Mdachi amesema kuwa wazazi tupunguze ubize tuwaoshe na tuwakague watoto wetu mara kwa mara,tuache kuwaita watoto majina ya ajabu na fedhea,ulawiti ishakuwa kama mtindo wa maisha tuungane kupaza sauti kupinga haya mambo kwani hata vitabu vya dini vinakataza.”


Mhe.Stella Mlacha ni hakimu mahakama ya Ilemela (kituo jumuishi) amewahusia kina mama kutambua kuwa wao ndio walezi na walinzi wa familia na wazingatie malezi mazuri kwa watoto toka wakiwa wadogo kwa kuamini kuwa mtoto hatoweza kuacha njia iliyo sahihi kirahisi.


Akihitimisha kongamano hilo Mratibu wa masuala ya kupambana na ukatili Manispaa ya Ilemela Sarah Nthangu amewashukuru wadau wote na wanawake wa Ilemela walioshiriki   kongamano hilo huku akisisitiza wazazi kupunguza usiri katika masuala ya elimu ya uzazi kwa watoto na kuwafanya watoto kuwa marafiki ili wawe huru kusema chochote kinachowasibu .


Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.