• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

JAMII YA ILEMELA YATAKIWA KUTUNZA MAZINGIRA

Posted on: March 11th, 2023

Jamii ya Ilemela imetakiwa kutunza mazingira pamoja na kuwa na utamaduni wa kufanya usafi katika maeneo yanayowazunguka ili kujiepusha na magonjwa ya milipuko


Rai hiyo imetolewa na afisa mazingira wa manispaa ya Ilemela Bi Jonathan Nyabugumba wakati wa zoezi la kufanya usafi na utoaji wa elimu juu ya kutunza mazingira na urejeshaji wa taka ngumu katika mialo ya manispaa ya Ilemela ambapo amewataka wananchi kujenga utamaduni wa kusafisha maeneo yao wanayoishi pamoja na kutunza mazingira yanayowazunguka ili kujikinga na magonjwa yanayosababishwa na mazingira machafu kama vile kipindupindu na magonjwa ya tumbo


‘.. Tusipotunza mazingira yetu tutapatwa na magonjwa ya milipuko, Na huu ni wajibu wetu sisi wananchi sio mpaka Serikali itusimamie wapo mawakala katika maeneo yetu lakini na sisi tuna wajibu wa kufanya katika utunzaji wa mazingira ..’ Alisema

Aidha Bi Nyabugumba mbali na kuwashukuru wadau wa mazingira kutoka taasisi za chuo kikuu cha Dar es salaam, Arena recycling na Emedo ya jijini Mwanza amewataka wananchi kuendelea na utamaduni wa kufanya usafi hata baada ya taasisi hizo zinazotoa elimu ya mazingira kumaliza muda wao wa kazi ndani ya Ilemela pamoja na kusisitiza mawakala wa usafi kutekeleza wajibu wao katika maeneo yao ya kazi


Bahati Mayoma ni mhadhiri kutoka chuo kikuu cha Dar es salaam shule ya sayansi akua na teknolojia ya uvuvi, yeye amewataka wananchi kutunza mazingira ya fukwe za ziwa viktoria ikiwa ni pamoja na kuhakikisha hakuna uingizaji wa plastiki ndani ya ziwa hilo, utekelezaji wa shughuli za kibinadam kando ya vyanzo vya maji sanjari na kuziasa BMU kusimamia wajibu wake ikiwemo usafi wa ziwa na mazingira yake pamoja na kubainisha tafiti mbalimbali zinazoelezea juu ya namna ziwa viktoria na mazalia yake vinavyoathiriwa na uharibu wa mazingira

Khamis Masimba ni mjumbe wa Serikali ya mtaa wa Mihama na January Lucas ni mwenyekiti wa BMU ya mwalo wa Igombe wote kwa pamoja wameshukuru kwa elimu iliyotolewa ya utunzaji wa mazingira na urejeshwaji wa taka ngumu huku wakiahidi kuwasimamia wananchi wenzao katika kuhakikisha mazingira yanatunzwa na kulindwa


Elimu juu ya utunzaji wa mazingira na urejeshaji wa taka ngumu imetolewa na taasisi ya ARENA kwa kushirikiana na chuo kikuu cha Dar es salaam kwa wananchi na viongozi wa mialo ya Kirumba, Mihama, Igombe na Kayenze ndani ya manispaa ya Ilemela kwa lengo la kupunguza athari za mabadiliko ya tabia nchi, uharibifu wa mazingira na kuzuia magonjwa ya mlipuko yanayosababishwa na mazingira machafu.



Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.