• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

ILEMELA YAWATAMBUA WANAWAKE JASIRI

Posted on: March 6th, 2025

Kuelekea maadhimisho ya siku ya wanawake ya kimataifa ,Wilaya ya Ilemela imekutanisha makundi mbalimbali ya wanawake  kupitia hafla ya Usiku wa mwanamke uliowakutanisha makundi mbalimbali ya wanawake wa Ilemela maalum kwa ajili ya kutambua michango ya wanawake katika jamii ya Ilemela kwa kutoa tuzo za pongezi.

Akikabidhi tuzo kwa wanawake walionyesha kufanya kazi kubwa na kuwa msaada kwa wengine kwa namna tofauti tofauti kwa viwango vya juu Katibu tawala wa Wilaya ya Ilemela wakili Mariam Msengi akimwakilisha Mkuu wa Wilaya ya hiyo amesema ni wakati wa wanawake wote kuungana na kutambua kazi zinazofanywa na wengine ,kuondoa chuki baina yao na kujenga utamaduni wa kusaidiana kufikia malengo waliojiwekea .

“..Tunatambua juhudi kubwa zinazofanywa na wanawake katika masuala mbalimbali ya kiuchumi,malezi katika familia.Wanawake ni jeshi kubwa na tuna nafasi ya kufanya mambo makubwa yenye tija kwa umoja wetu..”

Prisca Mkungu mmiliki wa kampuni ya Jimap Cleaning Services Company Ltd ni miongoni  mwa  wanawake waliopata tuzo za pongezi kwa kuwa mwanamke jasiri kwa kutoa fursa za ajira kwa wanawake wenzake ambapo zaidi wanawake 15 wameajiriwa kwenye kampuni hiyo.

Wakili Msengi ameongeza kuwa ni wakati wa kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muuungano wa Tanzania Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kazi nzuri anayoendelea nayo ya kuleta maendeleo kwa kila mwanamke kuitendea haki nafasi aliyo nayo katika jamii huku akianisha uwepo wa miradi mikubwa ya sekta ya elimu,afya na miundo mbinu inayoendelea kutekelezwa Ilemela.

Nae Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela Bi.Ummy Wayayu amesema kuelekea maadhimisho ya siku ya wanawake duniani Manispaa yake kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wameweza kufanya shughuli za kijamii kwa kutoa misaada mbalimbali kwa wahitaji na kutembelea wagonjwa wa kansa katika hospitali ya Rufaa Bugando huku akiwashukuru wadau hao kwa kufanikisha tendo hilo lenye baraka .

“.. Namshukuru Rais wetu Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kutambua nafasi ya mwanamke kwa kutoa nafasi nyingi za uongozi kwa wanawake,na pia nampongeza kwa kurudisha mikopo ya asilimia 10 ya mapato ya ndani ambayo kwa awamu ya kwanza tayari tumetoa shilingi milioni 618.6 kwa vikundi 39 vya wanawake.Naamini mtarejesha vizuri ili zoezi liwe endelevu na wengine wapate..”

Tumsifu Matutu ni mkazi wa kata ya Kawekamo yeye ni mzungumzaji wa kutia moyo amesema ni muhimu kutambua mipango uliyojiwekea ya kufanikiwa katika maisha na kuwataka kina mama hao kutokuzipa nafasi changamoto za kimaisha kuwazuia kufikia malengo huku akisisitiza upendo baina yao.

Jumla ya tuzo kumi zimetolewa kwa wanawake vinara wanaojishughulisha na ujasiriamali ,biashara na utumishi wa umma.








































Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.