• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

ILEMELA YATAKIWA KUZINGATIA MATUMIZI SAHIHI YA TAKWIMU

Posted on: October 13th, 2023

Viongozi na watendaji wa Manispaa ya Ilemela wametakiwa kuzingatia matumizi sahihi ya takwimu ili kufanya maamuzi  kwa utashi wa kitakwimu kwani serikali imewekeza fedha nyingi katika zoezi la sensa

Rai hiyo imetolewa na Ndugu Omary Mdoka, mkufunzi wa mafunzo ya usambazaji na matumizi ya matokeo ya sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 kwa viongozi na watendaji wa halmashauri ya manispaa ya ilemela

“Takwimu hizi ziwe chachu ziwe muongozo katika kutekeleza miradi mbalimbali kupanga mipango  sambamba na utungaji wa sera”, alisema ndugu omary


Nae Ndugu Benedict Charles Mugambi, ambae ni meneja idara ya shughuli za kitakwimu Na Mkuu Wa Sehemu Ya Gis kutoka ofisi ya taifa ya takwimu akimwakilisha Mtakwimu Mkuu Wa Serikali amesisitiza juu ya matumizi ya matokeo ya senda katika masuala yote yanayopangwa kutekelezwa kupitia muongozo wa matumizi ya matokeo ya sensa uliotolewa na mhe rais


“Kazi yetu sisi ni kuwaonyesha namna ambavyo mnaweza kutafsiri matokeo ya sensa na ambavyo mtayatumia katika mipango mbalimbali”, alisema ndugu benedict


Matokeo ya sensa ambayo yametolewa hadi sasa na yamezinduliwa yamefanyiwa uchambuzi hadi ngazi ya kata /shehia lengo kikiwa ni kufika katika ngazi za mitaa na vitongoji hii ni miongoni mwa jambo linaloifanya sensa ya watu na makazi kuwa  ya kipekee,




Akifungua mafunzo hayo Mhe Hassan Masala, Mkuu Wa Wilaya Ya Ilemela alisema kuwa Ilemela imejipanga kuhakikisha mipango na programu zote za maendeleo zinapangwa kwa kuzingatia matokeo ya sensa ya watu na makazi, sensa ya majengo na sensa ya anwani za makazi ya mwaka 2022.


Wakichangia katika mafunzo hayo wenyeviti wa mitaa ya manispaa ya ilemela katika nyakati tofauti wameomba matokeo haya ya sensa yakatumike katika kupatikana ramani sahihi za maeneo yao ili ziweze kusaidia katika matumizi mbalimbali


Mwakilishi wa kundi la walemavu ameomba serikali kupitia ofisi ya mkuu wa wilaya kuangalia shule ambazo zina elimu jumuishi ili ziweze kusaidia watoto wenye ulemavu waweze kupatiwa vipaumbele katika kupata elimu iliyo bora ili ikawapunguzie makali ya ulemavu.


Sambamba na mafunzo hayo, ofisi ya Taifa Ya Takwimu, ilikabidhi ramani ya manispaa ya Ilemela ikionyesha idadi ya watu kwa kata, pamoja na ramani za kwenye kata zikionyesha mgawanyiko wa watu na idadi yao kwa kila kata.

Kwa mujibu wa matokeo ya sensa, halmashauri ya wilaya ya ilemela ina idadi ya watu 509,687 kutoka watu 343,001 mwaka 2012. Kati ya idadi hiyo, watu 241,137 ni wanaume na watu 268,550 ni wanawake. Aidha, idadi hiyo inaonesha kiwango cha kasi ya ukuaji wa idadi ya watu katika manispaa yetu katika kipindi cha miaka kumi iliyopita yaani kutoka mwaka 2012 hadi 2022 ni wastani wa asilimia 32


Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.