• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

ILEMELA YAPONGEZWA USHINDI WA MPIRA WA KIKAPU SHIMISEMITA 2024

Posted on: September 6th, 2024

Timu ya mpira wa kikapu ya wanaume ya Halmashauri ya manispaa ya Ilemela imepongezwa kwa ushindi  baada ya kuifunga Timu ya halmashauri ya wilaya ya Iringa vikapu 49 kwa 44 katika hatua ya fainali iliyochezwa katika viwanja vya chuo cha ualimu Butimba jijini Mwanza


Akizungumza wakati wa kufunga mashindano hayo katika uwanja wa mpira wa miguu wa Nyamagana, Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mhe Said Mtanda amesema kuwa mashindano ya shirikisho la michezo serikali za mitaa Tanzania SHIMISEMITA  yamekuwa na faida nyingi kwa watumishi ikiwemo kujenga afya, kujenga ukakamavu, weredi, umoja, upendo na mshikamano miongoni mwao sanjari na kuwa Kama sehemu ya kuunga mkono juhudi za Rais   Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan katika kukuza michezo


'.. Nitumie jukwaa hili ninawapongeza watu kutoka Ilemela kwa kupata ushindi katika michezo kadhaa, Mmekuwa mfano mzuri, Mmekuwa wenyeji wema ukilinganisha na wenzenu wa Mwanza jiji ninaamini watajifunza kutoka kwenu ..' Alisema


Aidha Mhe Mtanda amempongeza mwenyekiti wa shirikisho hilo kwa kuleta michezo hiyo mkoa wa Mwanza kwa kuwa Mwanza ndio kitovu cha michezo mbalimbali nchini huku akiwaagiza wakurugenzi kujipanga vizuri kwa mwaka mwengine wa mashindano hayo yatakayofanyika mkoa wa Tanga sanjari na kuwasisitiza wananchi kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa Kama kauli mbiu ya mashindano hayo inavyosema ya Shiriki uchaguzi wa serikali za mitaa kwa taifa endelevu



Kwa upande wake nahodha wa Timu ya mpira wa kikapu ya wanaume halmashauri ya manispaa ya Ilemela Ndugu Mponjoli Pheston Basalile amefafanua kuwa mchezo wao dhidi ya Iringa haukuwa mwepesi na kwamba kilichowasaidia kupata ushindi ni makosa madogo madogo ya wapinzani wao pamoja na Timu yake kuzidisha umakini, umoja, kujituma na mshikamano Kama kauli mbiu ya wilaya hiyo inavyosema hivyo kujituma na kuongeza bidii na baadae kupata ushindi huku akiahidi kuendelea kufanya mazoezi zaidi na kujiandaa kwa mwakani ili waendelee kubaki na ushindi huo kwa siku zijazo



Nae afisa michezo wa manispaa ya Ilemela Mwalimu Kizito Bahati Sosho akafafanua kuwa mchezo wa mpira wa kikapu haukuwahi kuwepo tangu kuanzishwa kwa mashindano hayo nakwamba manispaa ya Ilemela inakuwa ya kwanza kushinda kipengele hicho huku akiongeza kuwa hata katika michezo mengine manispaa yake ilikuwa ikifanya vizuri isipokuwa makosa madogo madogo ndio yaliyowafanya wakakosa ushindi na kwamba watajirekebisha ili wafanye vizuri katika mwaka mwengine huku akimshukuru mkurugenzi wa Ilemela Bi Ummy Mohamed Wayayu kwa kuunga mkono Timu yao kuanzia mwanzo mpaka tamati ya mashindano hayo


Mashindano ya shirikisho la michezo serikali za mitaa Tanzania SHIMISEMITA yalianza mapema Agosti 25, na kufikia tamati Leo hii Septemba 05, ambapo halmashauri mia moja zimeshiriki zikichuana kupata mshindi wa michezo mbalimbali ikiwemo bao, karata, mpira wa miguu, mpira wa wavu, mpira wa kikapu, kuvuta kamba, pool table na mpira wa mikono


Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.