• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

ILEMELA YAPONGEZWA NA NAIBU KATIBU MKUU OR-TAMISEMI

Posted on: July 29th, 2019

Naibu Katibu Mkuu OR-TAMISEMI Ndugu Tixon Nzunda, ameipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela kwa utekelezaji mzuri wa miradi katika sekta ya elimu kwani majengo yote aliyoyakagua yanaendana na thamani ya fedha  iliyotolewa


Pongezi hizo alizitoa jana tarehe   28.07.2019 alipokuwa katika  ziara ya kikazi katika Manispaa ya Ilemela kwa lengo la kukagua utekelezaji/ukamilishaji wa ujenzi wa miundombinu katika sekta ya elimu Msingi na Sekondari kupitia fedha zilizotolewa na OR-TAMISEMI kwa ajili ya ukamlishaji wa maboma kattika shule za sekondari pamoja na fedha za EPFR (fedha zinazotolewa kulingana na matokeo).

Ndugu Nzunda alisema kuwa amefurahishwa na namna ambavyo thamani ya fedha inaonekana katika majengo  yaliyyojengwa kupitia fedha iliyotolewa na serikali.Alitoa kauli hiyo alipokuwa akikagua ujenzi wa madarasa na bweni la wasichana katika shule ya sekondari ya Buswelu na kuwataka wakurugenzi wengine kuiga mfano huo hasa katika kuhakikisha wanajenga mabweni ya wasichana  katika shule za sekondari.

Aidha Ndugu Nzunda akiwa katika ziara hiyo aliweza pia kuongea na walimu na wanafunzi na kuwapongeza walimu kwa juhudi wanayoionesha katika ufundishaji huku akiwataka wanafunzi kusoma kwa bidii ili waweze kufaulu lengo ikiwa ni kurudisha heshima katika shule za umma.Huku akiwataka wanafunzi kuhakikisha wanasoma kwa bidii na kuwa na nidhamu kwani ndio msingi wa  mafanikio.

Aliongeza kwa kusisitiza kuwa, kila mwalimu afundishe masomo anayotakiwa kufundisha pamoja na kuhakikisha wanaongeza viwango vya ufaulu. Pia aliwasihi walimu kufanya kazi kwa upendo na kushirikiana huku akiwakumbusha kufanya shughuli za uwekezaji ili kuweza kujikwamua kiuchumi.


Sambamba na hayo amewashukuru walimu kwa kutokumwangusha kwa kufanya matumizi mazuri ya fedha katika ujenzi wa madarasa hayo na kuwataka kuhakikisha wanayatunza hayo majengo  ili yaweze kudumu kwa muda mrefu ili vizazi vingine navyo vije  vitumie.


Pamoja  na hayo amewaagiza viongozi wa sekta ya elimu kuanzia ngazi ya Mkoa,Wilaya pamoja na waratibu elimu kata kuhakikisha kuwa wanasimamia utekelezaji wa  mtaala wa elimu pamoja na kutambua kazi nzuri   zinazofanywa na walimu.


Nae Mkurugenzi John Wanga akipokea pongezi hizo amemuahidi Naibu Katibu Mkuu OR-TAMISEMI kuwa atatekeleza yale yote aliyoyaagiza  kwa kuhakikisha kuendelea kusimamia kikamilifu sekta ya elimu pamoja na sekta zingine na pia alimshukuru kwa kujitolea kwake kuwa mlezi wa shule ya Sekondari ya Buswelu.


Halmashauri ya Manispaa ya ilemela katika mwaka 2019, upande wa Elimu msingi ilipokea fedha za EP4R kwa mwaka 2019 kiasi cha Tsh.175,00,000.00 kwa ajili ya ukamilishaji wa vyumba 14 va madarasa huku kwa upande wa elimu sekondari kwa mwaka 2018/2019  ilipokea kiasi cha Tsh.  125,000,000 kwa ajili ya ukamillishaji wa maboma kumi ya vyumba vya madarasa katika shule tano  ambazo ni Buswelu,Nyasaka,Nyamanoro,Bujingwa  na Kisundi.



Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.