• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

ILEMELA YAPOKEA MSAADA WA VITANDA KUTOKA KOICA

Posted on: August 31st, 2023

Halmashauri ya manispaa ya Ilemela imepokea msaada wa vitanda kumi vya kisasa vitakavyotumika kwenye wodi ya wazazi ya kituo cha afya cha Buzuruga vyenye jumla ya thamani ya kiasi cha dola za kimarekani elfu nne sawa na shilingi za kitanzania milioni tisa na laki tano kutoka kwa shirika la maendeleo la watu wa Korea (KOICA) kwa kushirikiana na jumuiya ya wanafunzi waliosoma nchini humo inayojulikana kama KOAT


Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo yaliyofanyika katika viwanja vya kituo cha afya Buzuruga, Mwakilishi mkazi wa shirika la Korea nchini (KOICA) Bwana Manshik Shin mbali na kuishukuru jumuiya ya watu waliosoma Korea kwa kuratibu tukio hilo amesema kuwa anatambua changamoto zinazoikabili nchi ya Tanzania na kwamba Serikali ya Korea itaendelea kushirikiana na Tanzania kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu hivyo kinachofanyika sasa ni moja ya utatuzi wa kero hizo


‘.. Niombe uongozi wa kituo cha afya Buzuruga na manispaa ya Ilemela kwa ujumla wake kupokea mchango wetu, Mchango huu umetoka kwa watu wa Korea na Serikali yao kwa lengo la kutatua changamoto za wananchi kama sehemu ya ushirikiano wetu ..’ Alisema


Aidha Bwana Shin ameongeza kuwa msaada uliotolewa utaenda kupunguza changamoto zilizokuwepo japo kwa uchache huku akiahidi kuendelea kuona namna bora ya kushirikiana katika kumaliza kero zilizobaki zinazokabili wananchi


Kwa upande wake Rais wa jumuiya ya wanafunzi waliosoma nchini Korea (KOAT) Dkt Deman Abdi Yusuf amefafanua kuwa wamekuwa wakishirikiana na shirika la KOICA kutoa msaada katika nyanja mbalimbali zenye uhitaji nchini huku akitolea mfano msaada kama huo uliotolewa katika kituo cha afya Kurasini, ujenzi wa kituo cha damu salama cha kisasa jijini Dodoma, hospitali ya Muhimbili tawi la Mloganzila hivyo kuwaalika wa Tanzania kujiunga na jumuiya hiyo kwa kuwa inagusa maisha ya wengi na nchi kwa ujumla


Nae mganga mkuu wa kituo cha afya Buzuruga Daktari William Tinginya amesema kuwa licha ya kituo hicho kuhudumia wananchi wengi mpaka wa kutoka nje ya wilaya bado kinakabiliwa na upungufu wa vifaa tiba ikiwemo vitanda 32 licha ya leo kupokea vitanda 10, upungufu wa watoa huduma za afya wakiwemo madaktari, manesi na wataalam wengine wa afya hivyo kuomba shirika hilo na wadau wengine kuendelea kuona namna bora ya kukisaidia kituo hicho ili kiendelee kutoa huduma bora kwa wananchi.


Akitoa neno la shukrani Mstahiki Meya Wa Manispaa ya Ilemela Mhe Renatus Mulunga mbali na kuwapongeza wadau hao wa maendeleo, amewahakikishia ushirikiano kutoka katika manispaa anayoiongoza na kwamba Serikali peke yake haiwezi kumaliza changamoto zote zinazokabili wananchi bila ushirikiano kutoka kwa wadau wengine wa maendeleo

Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • WANANCHI 780 WAFIKIWA NA KLINIKI YA HUDUMA ZA MAENDELEO YA JAMII

    May 13, 2025
  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.