• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

ILEMELA YAPOKEA MADAWATI 170 NA MITI 1700 KUTOKA DESK & CHAIR FOUNDATION

Posted on: December 6th, 2023

Katibu tawala wa Wilaya ya Ilemela Adv.Mariam Msengi kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe.Hassan Masala amepokea jumla ya madawati 170 yenye thamani ya takriban shilingi millioni 11.9 na miti 1700 kutoka kwa mdau wa maendeleo taasisi isiyo ya kiserikali ya Desk & Chair Foundation.

Akizungumza wakati wa hafla ya mapokezi hayo Adv.Msengi amesema madawati hayo yamekuja kwa wakati muafaka kupunguza changamoto ya upungufu wa madawati uliopo katika baadhi ya shule ndani ya Manispaa ya Ilemela.

"Tunashukuru sana kwa msaada huu kwani inaonyesha tupo pamoja na serikali ya awamu ya sita katika kuindeleza sekta ya elimu ,wote ni mashahidi kwa fedha nyingi zinazoendelea kuletwa na Mhe.Rais za miradi ya Boost na Sequip kwa ajili maboresho katika shule zetu."

Aidha Mwenyekiti wa taasisi hiyo Sibtain Meghjee ametoa taarifa ya utendaji kazi huku akisisitiza utaratibu wao wa kuhamasisha jamii utunzaji wa mazingira kwa kutambua kuwa utengenezaji wa madawati unatumia miti hivyo ni lazima miti ipandwe kwa wingi zaidi kwa kuwa bado vizazi vinaendelea.

" Ni utaratibu wetu kila tunapotoa madawati ni lazima tupande mingine,kila dawati tunatoa miti 10.Hii ni kwa faida ya vizazi vya sasa na vijavyo."

Nae Mwenyekiti wa kamati ya huduma za uchumi ,afya na elimu wa Manispaa ya Ilemela Mhe.Hussein Magela diwani wa kata Ibungilo kwa niaba ya mstahiki Meya wa Manispaa hiyo amewapongeza taasisi hiyo kwa kazi nzuri wanazofanya za kusaidia jamii.

"Kwa sisi tunaoamini Mungu kazi hii mnayoifanya ni ya kumcha Mungu, watoto wetu watasoma vizuri mafanikio yao sio yao tu bali ni ya jamii nzima."

Mwakilishi wa madiwani wa Manispaa hiyo diwani wa kata ya Kitangiri Mhe.Donald Ndalo amesifu utaratibu wa taasisi ya desk and chair foundation kuona mbali zaidi kwa kutoa madawati na miti kwa maana ya kuongeza miti zaidi .

Leah Cosmas ni mwanafunzi katika shule ya msingi Kaserya yeye anashukuru kwa madawati hayo na kuahidi ufaulu mzuri.

Akihitimisha hafla hiyo kaimu Mkurugenzi wa Manispaa Mwl.Marco Busungu amewataka waalimu wote wa shule za msingi waliokabidhiwa madawati hayo kuyatunza na maeneo yote miti inakoenda kupandwa kusimamiwa vizuri isiharibiwe na tija yake ikaonekane .

Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.