Halmashauri ya manispaa ya Ilemela imekidhi vigezo vya kutekeleza miradi minne kati ya tisa iliyowasilisha kupitia mradi wa Green and Smart Cities Sasa chini ya ufadhili wa umoja wa ulaya.
Hayo yamebainishwa mara baada ya kupokea matokeo ya uchambuzi wa miradi mikubwa ya maendeleo iliyoambatana na wa majadiliano ya tathmini ya awali ya mnyororo wa thamani wa chakula ( food value chain) na mfumo wa kibiashara ( trade systems) yenye lengo la kuboresha mnyororo wa thamani wa chakula na mfumo wa mazingira ya kibiashara katika manispaa ya Ilemela.
Taarifa ya tathmini hiyo iliwasilishwa na kampuni ya triple line ya nchini Uingereza ambayo ilipewa kandarasi hiyo na shirika la maendeleo la Ufaransa (AFD) ambalo litafadhili miradi hiyo kupitia program ya Green and Smart Cities sasa inayo itakayo tekelezwa katika manispaa ya ilemela chini ya ufadhili wa umoja wa ulaya.
Kutokana na vigezo vilivyo ainishwa na AFD kwamba ili mradi uweze kupita inapaswa uwe na mchango wa kiuchumi (uzalishe mapato) na pia uweze kutoa fursa kubwa ya ajira; Hivyo kutokana na tathmini hiyo, miradi minne ambayo imekidhi vigezo ni pamoja na mradi wa Uboreshaji wa mwalo wa old igombe, Uboreshaji wa mwalo wa new igombe, Uboreshaji wa soko la samaki la mwaloni pamoja na Ujenzi wa soko la kisasa la buswelu.
Naye mwakilishi wa Ofisi ya Rais TAMISEMIi katika kikao hicho Ndugu Shaban Ghuhia ameshukuru kwa ushirikiano ulioonyeshwa na menejimenti ya manispaa ya ilemela katika utekelezaji wa kazi hiyo ambayo imechukua takribani miezi sita tangu june 2022 hadi desemba 2023. Huku akiahid kuendeleza ushirikiano wa dhati ili katika kusukuma mbele gurudumu la maendeleo ya wana ilemela na watanzania kwa ujumla.
Mradi wa Soko la Buswelu tumeutembelea tena na tumekubaliana kwamba utakuwa mkubwa na utahusisha ujenzi wa soko, ring roads kuzunguka soko na ujenzi wa kituo cha daladala kilichopo pembezoni mwa soko/ mkabala na sheli ya ASHICO na kuweka taa za barabarani kuzunguka soko alisema ndugu Nicos Papachristodoulous ambae ni Mkuu wa maendeleo jumuishi kutoka Kampuni ya Triple line
Wataalam kutoka kampuni ya Tripple line walihitimisha kwa kusema kuwa taarifa ya miradi hiyo itawasilishwa AFD na hatua ya kuja kwa mtaalamu wa kufanya upembuzi yakinifu itafuata.
Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
Postal Address: 735 MWANZA
Telephone: + 255 736 200910
Mobile:
Email: md@ilemelamc.go.tz
Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.