• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

ILEMELA YAENDELEA KUPATA HATI SAFI, RC MTANDA APONGEZA

Posted on: June 26th, 2024

Katika kipindi cha miaka mitano mfululizo halmashauri ya manispaa ya Ilemela imeendelea kupata hati safi (unqualified opinion), hayo yamesemwa na ndugu Athuman Mustapha mkaguzi mkuu wa nje alipowasilisha taarifa ya hesabu zilizokaguliwa na mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali (CAG) katika kipindi cha mwaka wa fedha 2022/2023 kwenye mkutano maalum wa baraza la madiwani uliofanyika tarehe 26 Juni 2024 ukihudhuriwa na Mkuu Wa Mkoa Wa Mwanza Mhe. Said Mtanda.


Akiwasilisha taarifa hiyo Ndugu Mustapha amesema kuwa katika kipindi cha mwaka wa fedha 2022/2023 hoja 17 zimetekelezwa huku hoja saba zikiwa katika hatua za utekelezaji ambapo amezitaja baadhi ya sababu ya kutofutwa kwa hoja hizo ni kukosekana kwa baadhi ya vielelezo.

Nae Mhe Said Mtanda Mkuu Wa Mkoa Wa Mwanza, akizungumza na baraza la madiwani, ametumia nafasi hiyo kuipongeza Manispaa ya Ilemela kwa kuendelea kupata hati safi kwa miaka mitano mfululizo huku akimtaka mkurugenzi kuhakikisha anazifuta hoja zilizobakia ikiwa ni pamoja na kuwasilisha mpango kazi wa kujibu hoja zilizobaki katika ofisi ya Mkuu Wa Mkoa kupitia katibu tawala ifikapo tarehe 28 juni 2024.


“Pongezi nyingi kwa Manispaa ya Ilemela, kwa kuendelea kupata hati inayoridhisha (hati safi) kwa miaka mitano mfululizo, nyie mkipata hati safi maana yake msimamizi wa halmashauri ambae ni mkuu wa mkoa nae amefanya kazi nzuri”amesema mhe mtanda.


Aidha Mhe Mtanda ameutaka uongozi wa Ilemela kuendelea kutoa ushirikiano wa karibu kwa mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali (CAG) kwa hesabu za mwaka 2023/2024 ili kuweza kushughulikia hoja hizi kwa wakati na kuweza kufuta hoja zote



Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilemela, Mhe Renatus Mulunga kwa niaba ya baraza la madiwani amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa maelekezo aliyoyatoa na kumuahidi kuendelea kuwasimamia watendaji na kuhakikisha kuwa hoja zilizobaki zinakamilishwa kwa wakati.

Kwa mujibu wa sheria ya fedha ya serikali za mitaa (local government finance act 1982) iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2019, kila baada ya mwaka wa fedha kuisha halmashauri zinapaswa kuwasilisha taarifa zake za hesabu kwa mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali kwa ajili ya ukaguzi na baada ya ukaguzi halmashauri hupewa nafasi ya kujibu hoja


Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.