• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

ILEMELA YAENDELEA KUKABILIANA NA UTAPIAMLO KWA WATOTO

Posted on: October 13th, 2023

Katika jitihada za kutokomeza utapiamlo Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela kupitia kitengo cha lishe imeanzisha zoezi la ugawaji wa chakula lishe kwa watoto wenye utapiamlo mkali katika mitaa yote 171 inayounda Manispaa hiyo


Hilo limedhihirika katika zoezi la ugawaji wa chakula lishe kwa watoto wanaoishi katika Manispaa ya Ilemela lililongozwa na Bi Mariam Msengi ambae ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Ilemela.katika Kituo cha Afya cha Buswelu.


Akikabidhi chakula hicho kwa wazazi wa watoto hao, Bi Mariam Msengi ambae alimwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, amesema  kuwa Manispaa ya Ilemela inaunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya sita za uboreshaji wa  huduma za lishe kwa kutoa fedha katika sekta hiyo kwa kutambua umuhimu wa wananchi wote kuwa na lishe bora tangu wakiwa wadogo ili kuwa na nguvu kazi imara katika ujenzi wa taifa letu.


Sambamba na hilo Bi Mariam, amewapongeza wakina baba waliofika katika kituo cha afya Buswelu kwa ajili ya kupata huduma za kliniki pamoja na kusikiliza elimu ya lishe huku akiwasihi kina baba waliopo nyumbani kuhamasika na kutenga muda wa kuwa na watoto wao.


" Nawapongeza kina baba waliojitokeza hapa leo kuleta watoto wao kupata huduma za kliniki na pia kusikiliza elimu ya lishe inayotolewa na wataalam ni kitu kizuri na kinajenga upendo wa mtoto kwa wazazi wote wawili baba na mama.Kina baba wengine huko nyumbani mhamasike kutenga muda wa kuwa na watoto wenu kama hivi ."


Nae mwakilishi wa Mganga Mkuu wa Manispaa ya Ilemela Bi.Nyabwire Lukumai amesema kuwa Manispaa ya Ilemela kupitia idara ya afya inaendelea kuhamasisha  ushiriki wa kina baba katika huduma mbalimbali za uzazi ikiwa ni pamoja na kuwapeleka watoto wao kliniki.

" Mtoto ni wa wote hivyo kwa pamoja baba na mama wanawajibika katika malezi katika nyanja zote." Amesema Bi.Nyabwire


Akiwasilisha taarifa ya hali ya lishe Ilemela Bi.Pili Kassim amesema Halmashauri imeendelea kutenga kiasi cha shilingi 1000 kwa kila mtoto mwenye umri chini ya miaka 5 katika kuhakikisha watoto wote wanafikiwa kwa lengo la kupunguza na kutokomeza utapiamlo na kuendelea kuhamasisha jamii kulima mazao yenye viini lishe kwa wingi ili kuimarisha afya zao.

Bwana na Bibi Nzobana ni wakazi wa kata ya Kahama katika mtaa wa Buyombe wao wanaipongeza serikali kwa kuanzisha utaratibu wa ugawaji lishe sambamaba na utoaji wa elimu endelevu ya lishe kwa wananchi.


Nae Juma Alphonce ni mzazi wa Judith yeye ni mkazi wa kata ya Shibula anajivunia kuwa baba bora kwa kutoa huduma mbalimbali zinazohitajika kwa mwanae.


Kiasi cha Shilingi Milioni 7.45 kimetumika kununua chakula lishe hicho ambacho kimetolewa kwa watoto 40 wenye umri wa kuanzia miezi sita hadi miaka 5 wenye utapiamlo  mkali ambapo lengo ikiwa ni kuwafikia watoto 100 kwa kila robo ya mwaka




Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.