• Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
    • Malalamiko |
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL
ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government ILEMELA MUNICIPAL COUNCIL

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Idara
        • RASILIMALI WATU NA UTAWALA
        • MIPANGO NA UFUATILIAJI
        • ELIMU YA AWALI NA MSINGI
        • ELIMU SEKONDARI
        • KILIMO,MIFUGO NA UVUVI
        • VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI
        • MAENDELEO YA JAMII
        • MIUNDOMBINU NA UENDELEZAJI MIJI NA VIJIJI
        • AFYA USTAWI WA JAMII NA HUDUMA ZA LISHE
      • Vitengo
        • USIMAMIZI TAKA NA USAFI WA MAZINGIRA
        • MALIASILI NA UHIFADHI WA MAZINGIRA
        • MICHEZO UTAMADUNI NA SANAA
        • Fedha na Uhasibu
        • SHERIA
        • UKAGUZI WA NDANI
        • MANUNUZI
        • TEHAMA
        • MAWASILIANO SERIKALINI
    • Kata
      • BUGOGWA
      • BUSWELU
        • BUZURUGA
      • BUZURUGA
      • IBUNGILO
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Leseni
    • Usafi wa Mji
  • Baraza La Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • KAMATI YA FEDHA
      • KAMATI YA MIPANGOMIJI, UJENZI NA MAZINGIRA
      • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU
      • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI
      • KAMATI YA MAADILI YA MADIWANI
      • BODI YA VILEO
      • MFUKO WA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JIMBO (CDCF)
      • BODI YA AJIRA
      • ALAT
      • LVRLAC
    • Ratiba ya Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi iliyopendekezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Majarida
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Hotuba za Viongozi
    • Maktaba ya Picha
    • Video

ILEMELA YAANZA UTHAMINI KWA WANANCHI WENYE MIGOGORO YA ARDHI NA JESHI

Posted on: July 4th, 2019


Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela imeanza kutekeleza zoezi la uthamini kwa wananchi wake wa mitaa ya Lukobe na Buduku kata ya Kahama waliokuwa wanaishi katika mipaka ya Jeshi la wananchi wa Tanzania na kusababisha mgogoro mkubwa na wa muda mrefu kwa zaidi ya miaka kumi.


Akizungumza na wananchi waliojitokeza kuthaminiwa, Naibu waziri wa Wizara ya ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi ambae pia ni mbunge wa jimbo la Ilemela, Mheshimiwa Daktari Angeline Mabula amewatoa hofu wananchi hao pamoja na kuwataka kutolihusisha zoezi hilo na siasa kwa kuhakikisha wanakuwa watulivu na kutoa ushirikiano kwa wataalamu wa Wizara ya Ulinzi na Manispaa ili kuongeza ufanisi na kulifanikisha zoezi hilo kwa wakati na haki ili kila mmoja aweze kupata stahiki yake.

‘.. Niwaombe kuwa wavumilivu kwa masuala yote yenye uhitaji wa kisheria na yale ya maridhiano kati ya pande mbili, Hakuna mwananchi atakaepunjika, hakuna mwananchi atakaedhulumika na hakuna mwananchi mwenye haki atakaeachwa kikubwa kinachotakiwa ni kutoa ushirikiano ..’ Alisema


Aidha Daktari Mabula mbali na kuwashauri wananchi hao juu ya kufungua akaunti za Benki ameishukuru Serikali ya awamu ya Tano chini Rais Mhe Daktari John Magufuli kwa kusaidia wananchi wanyonge na Viongozi wa Wizara ya Ulinzi kwa kulipa kipaumbele jambo hilo kwa kutenga Bilioni 16 kwa migogoro yote ya ardhi nchi nzima huku Bilioni 3 na milioni 534 zikipelekwa mtaa wa Nyagungulu  kata ya Ilemela kuanza kulipa fidia wananchi wa mtaa huo baada ya kuisha kwa zoezi la uthamini na uhakiki.


Kwa upande wake kiongozi wa zoezi hilo kutoka Wizara ya Ulinzi, Luteni Kanali Mgugule amesema kuwa lengo la zoezi ni kuwafidia wananchi ili kupisha eneo la jeshi kwa sababu za kiusalama na kupunguza migogoro isiyokuwa ya lazima sambamba na kuwashukuru kwa kupokea vizuri zoezi hilo huku akiwahakikishia kutenda haki na kuwataka kuliamini jeshi lao.

Mwenyekiti wa mtaa wa Lukobe, Ndugu Paul Lameck ameishukuru Serikali na mbunge wa jimbo hilo kwa juhudi kubwa alizozichukua kuhakikisha wananchi wake wanapata fidia na kuumaliza kabisa mgogoro huo uliokuwa ukiwatesa kwa miaka mingi huku akiahidi kutoa ushirikiano ili kufanikisha zoezi hilo.


Kennedy  Chiguru ambae ni Afisa Mipangomiji kutoka manispaa ya Ilemela alisema kuwa Zoezi hili la uthamini ni la muda wa kipindi cha siku saba yaani kuanzia  tarehe  1-7 mwezi julai hivyo kuwataka wananchi kujitokeza katika maeneo yao na kutoa taarifa sahihi ili kupunguza changamoto zisizo za lazima.




Announcements

  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WENYE ULEMAVU April 28, 2025
  • TANGAZO MALIPO YA WALENGWA WA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI April 27, 2025
  • TANGAZO LA MWALIKO WA KUHUDHURIA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAANDISHI WASAIDIZI KUELEKEA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU AWAMU YA PILI April 27, 2025
  • TANGAZO LA UWEKEZAJI KWA MFUMO WA UBIA (PPP) December 04, 2024
  • Tazama zaidi

Habari mpya

  • RAI YATOLEWA KWA WAZAZI WENYE WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM

    May 05, 2025
  • MKURUGENZI UMMY ASISITIZA HUDUMA BORA ZA AFYA

    April 30, 2025
  • WANANCHI ILEMELA WAHIMIZWA KUHAKIKI TAARIFA ZAO KATIKA DAFTARI LA AWALI LA WAPIGA KURA

    April 30, 2025
  • WALENGWA TASAF WAASWA KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA VIKUNDI

    April 28, 2025
  • Tazama zaidi

Video

MAKALA MAALUM MIAKA 3 YA RAIS SAMIA UTEKELEZAJI WA MIRADI ILEMELA
More Videos

Quick Links

  • Mfumo wa ofisi mtandao
  • Mfumo wa Kieletronikio wa watumishi
  • Mfumo wa TAUSI
  • Vibali vya kutoka nje ya nchi
  • Salary slip

Related Links

  • Tovuti ya Serikali mtandao
  • Tovuti ya Ikulu
  • Tovuti ya utumishi
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Idara ya Habari maelezo
  • Tovuti ya Mkoa wa Mwanza

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

freevisitorcounters's Website

Location Map

Contact Us

    Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela

    Postal Address: 735 MWANZA

    Telephone: + 255 736 200910

    Mobile:

    Email: md@ilemelamc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Sitemap

Copyright ©2017 Ilemela Municipal Council . All rights reserved.